
Uwiiiiii, mpaka nimeumwa na tumbo la uzazi.....yani i just read this story kuhusu mtoto wa miaka 2
kung'atwa na mbwa wao mpaka akafa. Imagine alikuwa mbwa wa family for 8 long years.
yani this story hit home for me maana mie na mume wangu hapo ndo tunapokuwa hatuelewani.
Mume wangu anataka mbwa ili awe anacheza na Kenzo mie ndo staki kuona mbwa ndani kwetu maana nawaogopa balaaa...
mie vi puppy tu vinaweza kunifanya nipande juu ya makochi..lol..
I think ni jinsi nilivyokuwa, kwetu kulikuwa na mambwa 6, hayo mambwa yanafunguliwa usiku tu tukiingia kulala. Tena yalimzoea mlinzi wetu tu basi
anybody else yanaua, wezi walikuwa hawasogei nyumbani kwetu, hata sie wenyewe tulikuwa tunawaogopa balaa.
yani ilikuwa kama mtu umetoka out unaanza kuwaza hivi ntaingiaje nyumbani...hehehehehe
Yani this is all i know about dogs, kuwa ni wanaua sio wanyama wa kupeti peti.....
Sasa mume yeye ndo anapenda mbwa balaaaa....
Leo nilivyoona hii story yani ndo nimepata nguvu ya kumwambia, unaona?????
yeye mweneywe kaishiwa nguvu kabisaaaaaaa, kakaa kimya maana imagine ajali kama hii
mwanao aliwe na mbwa wako mpaka afe si utaokota makopo kwa kudata??? maana wanasema hakuna maumivu kama maumivu ya kuzika mwanao.
Yani huyo mama hapo pichani sijui ana hali gani. Maana bora mtoto aumwe au apate ajali, ila kuliwa na mbwa in your house , du????
unaweza kujilaumu mpaka siku unakufa.
Yani hii story imenikumbusha story ya mama wa kihindi Dubai, walikuwa wanakaa very close na kwetu, basi kashuka chini kumpandisha binti yake kwenye school
bus akamwacha her 5yr old son upstairs kalala. basi mtoto akaamka akaamka akaenda dirishani akawaona mamake na dadake chini akaanza kuwaita, mama mtu kuangalia juu
anamwona mwanae anachungulia dirishani akadata anamwambia mwanae atoke dirishani sasa sijui mtoto akazani anaitwa na mamake asiruke dirishani nini, toka ghorofa ya 8 sijui.
Mama mtu hakuongea na mtu, alipanda tu lifti watu wakajua anaenda ndani kwake kulia, huyo kafika kwake nae akajirusha dirishani alipojirushia mwanae....
Baba mtu alikuwa kazini, kufika home anakuta kabaki binti tu ,mama mtu na the son gone...
uwiiii, nililiaaaaa utadhani nawajua, nililia ka chizi....
Eeeh Mungu, tutunzie wanetu jamani......
kwa kusoma zaidi story ya mtoto aleuwawa na mbwa ingia humu
kusoma story ya huyo mama wa Dubai ingia humu.
nimeshangaa hiyo story bado ipo online hadi leo