19September

WHAT WOULD YOU DO WITH YOUR MONEY IF YOU EVER GOT THIS RICH??

 

 

Since sipendi kuwa surrounded by un-happy people.

IF I WAS AS RICH AS THEM FORBES 400 PEEPS EVERY ONE AROUND ME WOULD GET RICH AS WELL......

LIKE I WOULD BUY A FRIEND OR A RELATIVE A HOUSE FOR THEIR BIRTHDAY....REALLY IT'S JUST MONEY......LOL...

HUWA NASHANGAA SANA KUONA MTU TAJIRI ANA MAHELA ALAFU RAFIKI ZAKE MAKAPUPU, IM ALWAYS LIKE REALLY????

WHY NOT UPGRADE THEM TOO??? LOL.....


I SWEAR THE DAY I GET RICH (AND I KNOW I WILL) MY FAMILY AND FRIENDS WILL KULA BATA BALAAAAAAAA.........LOL



CHARITY, CHARITY ,CHARITY, CHARITY, CHARITY, I COULDNT STRESS THIS ENOUGH, THERES NO BETTER WAY TO THANK GOD THAN HELPING THOSE THAT HAVE NO ONE......

FROM A BUSINESS PERSPECTIVE CHARITY IS ALSO TAX DEDUCTABLE......SOOO HEY WHY NOT HELP OTHERS AND GET A TAX BREAK AT THE SAME TIME???

Comments (140)

  • Sugar Bum Bum

    Sugar Bum Bum

    19 September 2012 at 17:45 |
    yaani mange mimi ukoo wetu mzima wangekuwa matajiri..... maana kuanzia babu mpaka kitukuu ni kuwaendeleza tuuuu ningewasomesha,,,, ningeinvest everthing fot them aiseeeeee
  • c's mum!

    c's mum!

    19 September 2012 at 17:46 |
    worrrrrrddddddd myceo ! kama unazo u should empower wenzako na kuwafanya wawe kwenye level flan, but the problem is, hao matajiri huwa hawana marafiki maskini kama mimi! marafiki zao wanakuwaga rich pipo wenzao, we mange ngoja utajirikeeeeee, kufikia hiyo level yao, utakuwa na watu wa class yako, huwa inakuja automatically tu! wish them luck!!
    • Afro-Mdhungu

      Afro-Mdhungu

      21 September 2012 at 01:50 |
  • RESPONSIBLE WOMAN

    RESPONSIBLE WOMAN

    19 September 2012 at 17:48 |
    Well said mangeliciouscheers
  • DESPERATE HOUSE WIFE

    DESPERATE HOUSE WIFE

    19 September 2012 at 18:17 |
    I WILL SHELTER AND FEED ALL THE POOR CHILDREN OF THIS WORLD, SO HELP ME GOD!

    YES KUSAIDIA NDUGU NA MARAFIKI NI MUHIMU JAMANI. UKOO WANGU MZIMA NA WAMUME WANGU (THEY BETTER BE NICE TO ME THOUGH LOL) WILL LIVE JUST LIKE ME. [-O
  • Anonymous

    Anonymous

    19 September 2012 at 18:24 |
    Ni kuzidi kumuomba Mwenyezi Mungu azidi kukubariki maana haujui la kesho,kesho ni ya Mungu.
  • Anonymous

    Anonymous

    19 September 2012 at 18:24 |
    Ni kuzidi kumuomba Mwenyezi Mungu azidi kukubariki maana haujui la kesho,kesho ni ya Mungu.
  • Uturn Addict

    Uturn Addict

    19 September 2012 at 18:29 |
    INSHAALLAH ONE DAY I WILL BE RICH, VERY RICH..

    AND I PRAY TO ALLAH AENDELEE KUNIPA MOYO NILONAO SASA,,,
    SITAVUMILIA KUMUONA MTU WANGU WA KARIBU ANAPITIA MAISHA NAYOPITIA I SWEA,,

    TOKA NIKO MDOGO NILIKUA NIKIMUOMBA MUNGU NIWE TAJIRI ILI NITOE LIFT KWA WANAFUNZI SINCE NLIKUA NANYANYASWA NA MAKONDA NA HIYO KITU HAIJAWAHI CHANGE AKILINI MWANGU..

    I HAVE SO MANY DREAMS KUHUSU NIKIWA TAJIRI N I PRAY TO ALLAH ANIWEPESISHIE,,

    MANGE LEO UMEONGEA POINT NA UMENIGUSA SANA WALLAH,,

    SIELEWI HOW PEOPLE MANAGE TO BE HAPPY WHILE THEIR FAMILY AND FRIENDS ARE NOT....

    KUNA WATU WANA WEALTH YA KUTOSHA KUFANYA UKOO WAKE MZIMA KUISHI MAISHA YA KIFAHARI LAKIN WALA HAWAWAZI,,,

    MAY BE NAONGEA HIVI COZ I DONT KNOW HOW IT FEELS TO BE IN RICH PEOPLES SHOES,,,,,

    BUT............I L BE RICH AND INSHAALLAH I WILL SHARE MY WEALTH, MY MONEY..

    ONE DAY YES IF GOD WISHES,,
    • Mshamba

      Mshamba

      20 September 2012 at 20:11 |
      Umeandika vizuri sana Mungu akubariki uupate huo utajiri, U-turn addict. Tatizo lililopo hapa U-turn addict mtu akisema tajiri, ni kigezo gani kilichotumika (hao ambao wana US$10M kuendelea unaweza ukasema ni matajiri). Wengine wakiwa na TZS. 100M kwenye account anakuambia tajiri mwingine ana assets hata za US$4M anakuambia kuwa yeye si tajiri ni middle class wala sio upper class. Makundi ya watu tofauti yana maana tofauti wakisema fulani ni tajiri. Kwako ukipata kiasi gani utasema ni tajiri?
      Halafu pia omba kupata furaha, amani na afya bora katika maombi yako. Unaweza ukaupata utajiri na usiwe na furaha wala amani. Nimeyaona kwa wanawake wengine ikabidi nibadilishe maombi yangu kiujumla.goodluck
      • Afro-Mdhungu

        Afro-Mdhungu

        21 September 2012 at 02:12 |
        kiss umem'advise vizuri.
        Pesa inaraha yake kweli lakini kuna bitu binazidi pesa thamani...kama afya njema, mume awo mke bora, wazazi wema, familiya kuskilizana, kujipenda mwenyewe(not being insecure),kuwa na marafiki wazuri, kuwa nakazi ya kuweza ku stiri familiya....
        Watu wengi wenye pesa hawana marafiki wa ukweli, wengi wako juu ya interest i'm telling u unaweza kuwa tajiri lakini ukawa na stress kuliko asiyo kuwa tajiri, i know what i'm talking about some rich family are not the happiest one, ni paziya tuu mnaona material thing mnawaza ndiyo binafurahisha moyo?! Don't look only the outside of rich peaple...Ndani kwawo wengi wako na a lot of differents issues: a lot of infedelety, divorce, a lot of hypocrites around, hawana mda wakuwa pamoja na familiya, unakuta baba anatumika na mama anatumika wewe mtoto huwezi kupata mda wakuceza nawo yaani work agenda ziko full, mtoto anakuwa na kila kitu lakini wenye kumleya si wazazi wake, ikifika holiday ndo mna enjoy na familiya yote lakini ukiwa mdogo unaombaga wazazi wawe na kazi ya kawaida lakini mkuwe na mda wa kuwa wote kama familiya zingine...kila mtuu ana mtazamo wake wa kuwa tajiri lakini utajiri siyo ndo happiness BIG NO
        • Mshamba

          Mshamba

          21 September 2012 at 04:27 |
          • Muke Ya Albino

            Muke Ya Albino

            21 September 2012 at 12:53 |
            Umesema vizuri sana Mshamba na Afro mdhungu ni kweli where do we draw a line kwamba mtu akiwa na kiasi hiki ni tajiri??? same as poverty line. ni vigumu ku-difine utajiri na utajiri pia uko wa aina nyingi ingawa hapa nadhani tunazungumzia zaidi wa mali na pesa!! (hapa tuko kidunia zaidi).
    • basira

      basira

      21 September 2012 at 00:02 |
      uturn addict umesema kweli binafsi nna dada yangu mkubwa flani kwenye ccm hee huyo hashikiki kwa roho mbaya na uatajiri alionao haumithiliki lakini ndugu anatunyanyasa sana. anajali watoto wake tu . alimkataza hata mdogo wangu wangu mwengine asimlipie mtoto wangu private school na kweli mwanangu alitolewa hiyo skuli na kupelekwa local school. Baba amekufa hataki hata turithi chochote anakuwa mkali amecotrol yeye kila kitu.
      • sa

        sa

        21 September 2012 at 00:46 |
        pole dear lakini kwanini huyo mdogo wako asikusaide kumlipia ada mwanao kisirisiri,kwani mpaka mmwambia dada yenu kama unajua tabia yake ilivyo
        • Mshamba

          Mshamba

          21 September 2012 at 04:33 |
          SA nakubaliana na wewe kabisa. Kama huyo dada mwingine ana moyo wa kutoa na hataki kugombana na dada yake mkubwa aendelee kukusaidia bila kumwambia yeye. Sasa na wewe uweze kutafuta wa kumsingizia (kuwa umepata mfadhili mpaya) ili usimtie dada yako matatizoni. Hapo ndio ninakuwa sielewi kwa nini mtu mwingine amuingilie mwenzake uhuru wa kusaidia na wakati yeye sio mume au mke ambaye ana mamlaka ya kujadili pato la familia.
          • basira

            basira

            21 September 2012 at 11:21 |
            Huyo dada ni mkrofi sana amebrainwash baadhi ya ndugu na kusema kweli hata ameifanya famili igawike japo si amini uchawi lakini naona kama wenzangu wamezidiwa kwani hawawezi kufanya chochote bila ya kumwambia huyo dada. Hata hivyo nashkuru hiyo puplic school waliyomepeleka mwanangu kwa masimango,Mungu amemjalia amefaulu vizuri sana. Kinachonisikitisha tu kwa family kutengana kwani wazazi wote walishaenda mbele ya haki na huyo dada ndo kama mama ktk familia yetu. Nashkuru kwa ushauri mliyonipatia kwani angalau nimepata kutoa dukuduku langu.Nia yangu hasa ni kusupport maneno ya mange kwa kuwapa mfano hai nilionao kuhusu hao watu wanaojiweza wanavydhalilisha wenzao. Asante Mnage kwa kuleta topic hii
          • Muke Ya Albino

            Muke Ya Albino

            21 September 2012 at 12:57 |
            Pole sana Basira, nadhani huyo dada yako anasahau kuwa hapa duniani sote tunapita, na aliyempa yeye ndio huyo huyo kakunyima wewe!! usikate tamaa iko nawewe siku yako usimlilie binaadamu mwenzako hata siku moja wewe lia na Mungu wako tu.
      • Anonymous

        Anonymous

        21 September 2012 at 12:38 |
        Basira kwa nini mtoto wako usomeshewe na ndugu wewe huna mikono ya kuchakarika ukasomesha mtoto wako? unampa mtoto wako kitu kulingana na uwezo wako sio uwezo wa ndugu yako kwa hilo sikusapoti
        • sa

          sa

          21 September 2012 at 19:45 |
          we anonymous unasema tu naona hayajawahi kukukuta anaweza akawa pesa alizonazo ni kula na kulipa nyumba tu labda mshahara wake ni mdogo hautoshi kulipia private school sasa kama kuna ndugu zako wanauwezo wa kulipia private kuna tabu gani ya kusaidia ukiangalia ni elimu sio kwamba anaendatumbua pesa kwenye mambo yasiyo na maana.ninachukushauri basira omba msaada wa mtaji ufanye shughuli nyingine itayokuongezea kipato mbali na mshahara kama umeajiliwa tena mwendee huyo sister wako mwenye roho mbaya umpime tena.pole mwaya na kila la heri mungu atakusaidia
          • basira

            basira

            22 September 2012 at 03:37 |
            Nashkuru SA kwa ushauri wako mzuri, unaonekana ni mwenye busara na umekomaa kiakili. Kwa sasa kusema kweli sihitaji kuomba msaada wa mtaji wowote niko vizuri kimaisha, ila kwa huyo dada simrudii tena kwani ana hasira sana na mimi kuona nimeweza kusaidia mwanangu na wengine ktk famili na pia kuweza kuweka maisha yangu ktk standard ya kibinadam, hicho kitu kinamuuma sana na kwa vile baadhi ya watu wilioona mateso aliyompa mwanangu wanamsuta kwa macho kwa hiyo ni pigo kubwa kwake. Mungu akubariki ulichonacho akuongezee maradufu na akupe afya njema thanks
  • Uturn Addict

    Uturn Addict

    19 September 2012 at 18:31 |
    Au labda matajiri huwa wanaona bado time ya kushare na watu mpaka labda afikie leo ya utajiri ya hollywood lol
  • Uturn Addict

    Uturn Addict

    19 September 2012 at 18:35 |
    ila tusiwalaumu sana hawa matajiri..

    SOME TIMES SIO MAKOSA YAO AS YEYE ANAKUWA SO BUSY TO GET INTOUCH WITH EVERY ONE,,
    WHAT THEY DO IS THEY ASSIGN THAT TASK TO THEIR P.A OR MANAGERS TO FIND NEEDY PEOPLE IN DIFF ASPECTS,,,NA WANAWAPA PESA KABISA KWA AJILI YA HAO NEEDY PEOPLE....
    SASA WALE WATU BAADA YA KUWAFIKISHIA WALENGWA WANACHIKICHIA MIFUKONI MWAO.....

    WANAKUA WAMEPATA PESA YA HARAKA WENYEWE WANASEMAGA
  • Uturn Addict

    Uturn Addict

    19 September 2012 at 18:37 |
    KAMA HUYU OPRAH ANAENJOY VIPI LIFE JAMANI>............

    HANA HATA MTOTO WA KUSINGIZIWA BASI ANGEADOPT HATA TEN KIDS FROM THE POOREST COUNTRIES,,,,,,

    I LOVE MI SOME ANGELINA JOLIE N BRAD
    MADONA PIA,
  • Anonymous

    Anonymous

    19 September 2012 at 18:42 |
    NAONA KISWAHILI KINAKUPIGA CHENGA JAMANI NI " MAKAPUKU" SIO MAKAPUPU AU LABDA TYPING ERROR.
    JAMANI WOTE HAO 400 MUMEO HAYUMO?? MMH KWELI KAZI IPO, MASHAUZI YOTE HAYO JAMANI HAHAHAAAAA LOLEST, ANYWAY,YOU ARE RIGHT, NI VIZURI KUSAIDIANA ILA SABABU BINADAMU WENGI TUNA ROHO YA KWANINI, WATU NDIO MANA HATUSAIDIANI.
  • Muke wa muethiopia

    Muke wa muethiopia

    19 September 2012 at 18:43 |
    Wow...oprah knows how to put smile on pipo hearts over n over..just like my gal mange unamoyo wa huruma nakusaidia and thats the best kept secret to success..give and give and give na Mungu atakurudishia thousand folds...
  • Anonymous

    Anonymous

    19 September 2012 at 18:45 |
    mimi ningezipata hizo kwanza kabisa ningeacha kazi, nianzishe business 2 au 3 kubwa, niajiri watu, kazi yangu iwe kufuatilia tu. Sipendi kwenda kazini na kuwa bossed around, i swear maboss wa kibongo wanatesaga jamani, wanatunyanyasaje sasa? mtu nimesoma na kadegree kangu, na kamshahara kangu poa na ndugu wananiheshimu na kunitegemea lakini nikifika ofisini nawekwaje down jamani, naumiaga roho balaa.Kuna maboss wanaboa hadi hauna hamu ya kwenda kazini, anyway, nitajiendeleza niendelezee ndugu , jamaa na marafiki nao wasome, wafanye business etc Ila kikubwa kupita vyote namuomba mungu kama ntakuwa tajiri kiasi hiko NISIACHE KUWA NA HOFU YA MUNGU MAANA MATAJIRI WENGI SANA DUNIANI WAMEMSAHAU MUNGU, PESA INAWATIA KIBURI, INALETA USHETANI, MTU ANAMSAHAU MUNGU WAKE, HIYO SITAKI. Tunawaona watu wakishapata tu pesa ya kubadilisha mboga basi mungu ni pembeni hawana time, that is a BIG NO.
    • Anonymous

      Anonymous

      21 September 2012 at 11:17 |
      kweli kabisa
    • Muke Ya Albino

      Muke Ya Albino

      21 September 2012 at 13:01 |
      Ndio maana inasemekana "Ni rahisi ngamia kupenya katika tundu la sindano kuliko tajiri kuuona ufalme wa mbinguni"
  • Ti Vancouver

    Ti Vancouver

    19 September 2012 at 18:53 |
    Mange ubarkiwe kwa kuwa na mawazo ya aina hiyo Mungu akutimizie ahadi zako. Mi sijawahi kusahau huko kwetu ni kila mtu na watoto wake yaani hata kama baba mkubwa ni tajiri vipi hawezi kusaidia watoto wa ndugu yake.
    Anafurahi akiona mnateseka ili mzidi kumnyenyekea na kumwabudu kama mungumtu ndo awasaidie.
    Anyway Mungu amegeuza juu chini sasa ni baraka sana kusaidia wasio nacho kama ukibarikiwa. Mwingine anaona akikusaidia utapendeza kuliko yeye moyo wake unajaa furaha akiona unakongoroka tu. Nakuombea Kwa kuwa na moyo huo ufanikiwe kila unachopanga kufanya.
    Lakini labda uanze kuwa na marafiki hohehahe pia kwani naona marafiki zako wote mambo safi hawana shida wanakula good life chagua na wenye kipato kidogo pia uweze kuwainua.
  • Namsi

    Namsi

    19 September 2012 at 18:59 |
    Giving is coming from the heart and not how much you earn.There are billionnaire who are selfish.pray hard so that you can think about others so that you can have your reward thereafter.Inshallah Mungu atujaalie tuwe miongoni mwa wakumbukao kusaidia jamii Ameen
  • kiruuu

    kiruuu

    19 September 2012 at 19:00 |
    teammange ndo maana nakupenda unamawazo mazuri tofautigoodluck hivyo hivyo utafika mbali sanahakunaga kamamukeya
    mashauzi yanahitaji pesa ndiyo na upende kuendeleza wenzioooo ndugu jmaa n marafiki co kujitajirisha pekee yko ndo maana wengi we2 ha2endelei..
    ... mwishoo...
  • TILALILA

    TILALILA

    19 September 2012 at 19:03 |
    TAXI DEDUCTIBLE - ukimpa mtu kama zawadi u don't get to deduct on your tax and she/he doesn't get taxed on it.

    ukitoa kama charity lets say nyumba u get tax benefit and na huyo mtu inabidi alipie tax. hapo sasa tax imshinde! wengi wao wanashindwa kulipia tax wananyang'anywa

    so make sure watu wako wa karibu unatoa kama "gift" that way inakula kwako only
  • k0ku

    k0ku

    19 September 2012 at 19:17 |
    lmao kweli uyasemayoceo ila umesahau jambo moja ktk jamii zetu za kiafrika:hao hao wasio na uwezo ukianza kuupata huo utajiri ndio watakaokuwa wa kwanza kukusema unaringa kabla ya ile plan yako ya kutaka kuwatajirisha na wao- masikini mara nyingi wana vimaneno vya kajeri sana. pale unapoanza kuzishika hizo pesa tuu ndio matatizo ya ndugu utayajua hata kabla hazijajaa kwenye kibobo cha utajiri,mwisho wa siku wala ufikii kuwa kama OPERA..LOL..HUYU hana EXTENDED FAMILY ndio maana kajiwahia SA kuwekeza vyake vingineigaufe
    • Afro-Mdhungu

      Afro-Mdhungu

      21 September 2012 at 02:17 |
  • Uturn Addict

    Uturn Addict

    19 September 2012 at 20:37 |
    hahahahhahahah u truly mpare lolesh....

    ETI CHARITY IS TAX DEDUCTABLE
  • baby ya Mange

    baby ya Mange

    19 September 2012 at 20:39 |
    Baby bwana I can't think straight anymore akili yangu yote ipo kwenye CL na spike shoes!
    • Afro-Mdhungu

      Afro-Mdhungu

      21 September 2012 at 02:18 |
  • KIJACHO

    KIJACHO

    19 September 2012 at 20:48 |
    mange umenichekesha kweli eti your friend and family will kula bata ukiwa rich hahahaha any way kiukweli umenena CEO watu rich humu jamani tusaidieni na sisi ndio nini sasa hamtu upgrade wakati we are friends here in U TURN hahahaha.nasubiliwa ku upgradiwa na da CEO babu
  • baby ya Mange

    baby ya Mange

    19 September 2012 at 20:52 |
    Anyway if I ever get this rich I will first make sure av a roof for my family I mean my kids n my mom,sure of their good education,build them houses,open something like industry or any business which will keep the money coming!then I will open a charity centre I mean doing compassion, I will make sure I meet my dream girl I mean meet the people I love n dream of them like my baby here,,I will travel arround the world to see all wonders of the world,I will build one church build. Yeah
  • baby ya Mange

    baby ya Mange

    19 September 2012 at 20:59 |
    Baby don't forget baby ya Mange in ur kingdom,,,,as two or one year from now ur not gonna be same Mange!God bless ur heart my baby,,,mwuah!
  • kayemba ney

    kayemba ney

    19 September 2012 at 21:05 |
    blowkiss Tht is exact reson in to why I call ya a living angelthumbs up
  • kayemba ney

    kayemba ney

    19 September 2012 at 21:09 |
    Jamani mimi kwanza my family jaman uwiiiii,my good friends pia and charity Ofcourse!Hilo bata lake Uwiiii.Mashauzi Ndo yangenikoma coz napendajeee hahahahaha!Sema sashimi nimefyata matako as Nina za kuhesabu,mashauzi yataka pesalmao
  • kayemba ney

    kayemba ney

    19 September 2012 at 21:23 |
    Leo nafika ofcn wamefungia mange blog ukifungua unakutana na webmarshal this site is restricted,nikifungua mashuzi mengine yanafunguka.Daaah mekaa na mawazooo,muda wa lunch nilivorush home kufuata my iPad utasema nina mgonjwa ICU.Watajibeba km wametumwa vile.How can I spend the whole day bila kuingia huku!Watu wanasonyaje job na kuwachamba IT department hahaahaamangeblog
  • Cheerlicious Chick

    Cheerlicious Chick

    19 September 2012 at 21:44 |
    I believe you Mange. and i agree with you too!
    cheers
  • fanta

    fanta

    19 September 2012 at 21:48 |
    chary bwana sio lazima uwe tajiri kutoa ni moyo na si utajiriceo kwangu mimi we ni tajiri
  • Anonymous

    Anonymous

    19 September 2012 at 21:56 |
    Dada una mashauzi sana sidhani kama waweza kufanya walofanya kina Oprah, unachojua wewe nikwenda kununua na kuonyesha. Wenye navyo mara nyingi huwezi kuwajua. I am not hating you, freedom of speech
  • g.l.o.r.y.

    g.l.o.r.y.

    19 September 2012 at 21:59 |
    hili naamini coz ourceo sio mchoyo kbsa,
    u r very kindblowkiss
  • Anonymous

    Anonymous

    19 September 2012 at 22:06 |
    Mange kumbuka ni wewe ulipromis utafunga shindano ijumaa sasa wengine tunafanya kazi na familia mambo mengi, hebu tupe muda bwana. Kumbuka mshindi anaweza kupatikana leo au wa hiyo ijumaa tunaomba muda tafadhali. Afu ukichungua na kama walivyosema wadau hapo juu, walio wengi hawajafuata masharti please consiber that please.
    • Afro-Mdhungu

      Afro-Mdhungu

      21 September 2012 at 02:23 |
      laughing trueteller.com
      unajiteteya? We ni number ngapi...? lol
  • Uturn Addict

    Uturn Addict

    19 September 2012 at 22:35 |
    I LIKE IT WHEN UKIFATA USHAURI..

    HAYA WALE WA KUVOTE MARA MIA NANE DAWA YENU ISHACHEMKA NA NI CHUNGU KAMA SHUBIRI.....

    LOV U MK
  • Anonymous

    Anonymous

    19 September 2012 at 22:35 |
    Charity and more Charity
  • BORN TOWN

    BORN TOWN

    19 September 2012 at 23:22 |
    Huo wote ni uchoyo.utakuta mtu ni tajiri lakini ndugu zake masikini wa kutupwa au jirani yake kila siku analala njaa..by the way leo najipongeza kwa kufungua champagne maana nimekuwa wa kwanza.lolesh!
    • Uturn Addict

      Uturn Addict

      20 September 2012 at 19:03 |
      uwe wa kwanza utambe>//??????

      kuna watu wana mbio za marathon.......
    • Muke ya Muchina

      Muke ya Muchina

      20 September 2012 at 23:37 |
      rolling on the floorrolling on the floor Hahahaha tena nakuona shosti umekuwa wa kwanza loooool! uko mbele kama kitovu wala hukai nyuma....mbavu zangu mie UTURN ADDICTblowkiss
  • FAITH

    FAITH

    19 September 2012 at 23:27 |
    YEAH it is true Why not help others and get tax break and at the same time blessings from GOD
  • Anonymous

    Anonymous

    19 September 2012 at 23:49 |
    On this we are on the same page!Yaani....I so feel you.Dream big...if your dream is being a fundi cherehani(no disrespect to them) and you happen to be one...that's what you will be.But dream big...and your achievement will be big.
  • Anonymous

    Anonymous

    20 September 2012 at 00:23 |
    blowkissblowkissblowkissblowkissblowkissblowkiss for u mange
  • Anonymous

    Anonymous

    20 September 2012 at 00:24 |
    sonya sasa mahaters lol
  • Mshamba

    Mshamba

    20 September 2012 at 05:37 |
    I would have my Corporate and Social Responsibility (CSR) Department do the purchases and deliver to the shelters for Orphans, battered women and other types of shelters that are part of the Group vision and deliver the needed items (food, clothes, beds, and other requirements) themselves instead of money directly to the shelters. For access to education, medical and upgrading of shelter facilities these services can be hired directly by the CSR department to ensure that they know that their vision for the need is being realised.
    Yes, it would cost more money as you would have a bigger team but at the end of the day, the organization knows exactly what it has given and where the money is actually going and doing.
  • Mshamba

    Mshamba

    20 September 2012 at 06:00 |
    Mimi nina mtazamo tofauti kidogo kuhusu marafiki na kuwapa hela. Mimi naona kuwa na hela na kuwagaia marafiki/ndugu tu hivi hivi si msingi mzuri na kiujumla haitawasaidia hao marafiki/ndugu kama ambavyo wangeweza kuwasaidia. Ningekuwa tajiri kama kina Oprah (hata usifike kwa kina Bill Gates na Warren Buffet), marafiki/ndugu zangu ningewainua kwa kuwapa majukumu katika biashara zangu kutokana na vigezo walivyokuwa navyo. Kama hawana vigezo, kuna kazi zingine hata kutafuta watu mnaowataka kuwasponsor kwenye (CSR) hii inaweza kufanyika na mtu yeyote. Wakiwa na majukumu hawataona kama wanadharauliwa kwa kupewa tu hela kila siku ila watakuwa wana moyo wa kufanya majukumu hayo na kuupokea msaada kwa furaha kwa sababu ile hela wameitolea jasho na ni haki yao. Hata wanafamilia wa hao marafiki au ndugu (waume au wake, watoto na ndugu wengine) hawatawadharau hao marafiki/ndugu kwa kupewa tu kila siku. Kutakuwa na uendelevu wa pato (earnings continuity). Kwa mtaji huo hata mara moja moja ukiwapa zawadi ya nyumba kwenye birthday au tafrija nyingine yeyote una hakika kuwa atakuwa anaweza kuitunza ile nyumba na sio kutegemea tena uje kuitunza, chakula uwaletee, nguo uwavalishe na watoto uwasomeshe n.k.
    Kama wana uwezo wa kufanya biashara unawakopesha hela kama mtaji na kwa riba ndogo sana na riba ianze kulipwa wakati biashara imeshaanza na kujiendesha vizuri. Wao wataona kuwa hawajapewa tu hela ila wamekopa kama watu wengine wanavyokopa mtaji wa biashara (hata kama ile riba ni 0.1% kwa mwaka (p.a)) na ni juhudi zao wenyewe na kuwafanya wajiamini zaidi mbele ya jamii na wataweza pia kutunza familia zao na ndugu za familia zao kama wao pia wakihitajika kufanya hivyo na kuweza kuwasaidia watu wengi kiujumla (wazungu husema creating a ripple effect).
    • BEAUTIFUL ONYINYE

      BEAUTIFUL ONYINYE

      20 September 2012 at 19:35 |
      Well sayed..
      • Muke Ya Albino

        Muke Ya Albino

        21 September 2012 at 13:10 |
        Mshambacheers maana hao ndugu hupaswi kuwapa samaki bali unapaswa kuwapa nyavu wakavue... ndio wataona utamu wa samaki"
        • Mshamba

          Mshamba

          21 September 2012 at 22:22 |
          Muke ya Albino hicho ndicho haswaaa nilichotaka kusema. Ahsante kwa kuuleta huu mfano kumalizia point yangu!
    • Nai Nai

      Nai Nai

      20 September 2012 at 21:51 |
      blowkissblowkiss

      Mie sio tajiri lakini nilikuwa nafanya kama hivyo Mange anavyosema, matokeo yake watu wakawa wanaona wana rights kwenye pesa zangu na kutaka kunipangia wao.

      Nikabadili style ya kuwapa mitaji, matokeo yake mitaji yote imeliwa hakuna cha maana wala biashara inayofanywa. Yaani unampa mtu pesa wamwambia hizi lipia ada za shule, na hizi fanya mradi, lakini mwisho wa mwaka anakujia hana kitu you go back to square one.

      Sijui labda nikiwa tajiri ndio naweza kufanya hivyo tena lakini kwa sasa hivi I will deal with orphans lakini sio ndugu.
      • Mshamba

        Mshamba

        21 September 2012 at 04:48 |
        Hao ndugu wa kula pesa wapo kibao wakati huo utajiri hata huna pesa za kihivyo. Una hela tu za kujikimu na kufanya maendeleo kwenye maisha yako. Mimi cha kwanza nitasaidia elimu ya watoto wa ndugu wa karibu kwanza. Ningependa pande zote za familia mume na wadogo zangu elimu za watoto wetu zisipishane sana ili wote wawe sawa. Kwenye issue ya school fees kama ni hapa bongo nitakupa cheque uwapalekee au nitaomba account number kutransfer hela directly nikishajua kuwa hela unakula za school fees na mwanaye ambaye pia ni mwanangu (awe kwa wadogo zangu au kwa wadogo wa mume wangu). Tatizo ni huyu ndugu wala sio huyo mtoto asiyekuwa na hatia. Omba tu account namba ya shule uwe unapeleka moja moja kama bado una mpango huo wa kusaidia kwenye mambo ya shule.Kusaidia Orphans ni njia mojawapo nzuri sana.
      • muke ya jaluo

        muke ya jaluo

        21 September 2012 at 08:54 |
        NAI NAI NAONA THE BEST WAY SIO KUWAPA PESA LABDA UNAWEZA KUWATAFUTIA KOZI YEYOTE NA KUWAENDELEZA WALE WENYE INTEREST NA SHULE SABABU SHULE NDIYO JAMBO LA MSINGI AKIMALIZA ANAWEZA TAFUTA KAZI AU KUJIAJIRI MWENYEWE KAMA NINAVYOFANYA KWA NDUGU ZANGU
        • Nai Nai

          Nai Nai

          22 September 2012 at 04:42 |
          Dada wee acha tu, yote hayo nimefanya, wanatafuta kozi wenyewe, na wakati wanasoma unawalipia ada na kuwasupport kwa hali na mali, lakini mwisho wa siku hawamalizi hizo kozi. Ni mmoja tu so far ndio alijitahidi akamaliza. Hao ni ndugu ambao wanaona kwanini wahangaike wakati wewe unatosha kuhangaika. Hiyo mitaji ndio usiseme yaani unatoa kila kukicha matokeo nikajikuta kumbe mimi ndio nimefanywa biashara. Tatizo liko kwenye kuchange mindset ya watu ili waone kuwa wakisoma kozi fulani itawasaidia kusimama kwa miguu miwili. Sitaki kusema sana lakini kwa kweli inaumiza unajikuta wewe una sacrifice a lot ili tu mpunguze umaskini kwenye ukoo wenzio wanakuona unaringa au unajikomba.

          Kitu cha kushangaza sasa, ambao sio ndugu zangu na nimewapatia msaada kidogo tu (mie sina kipato kihivyo) japo wa mawazo yaani wako mbali sana, na ambao walitaka kulipiwa kozi tena za bei rahisi, sasa hivi wamemaliza kozi na kuajiriwa juu, I feel very proud na wanani inspire kutoa japo kidogo nilichonacho maana changes unaziona.

          Tatizo liko kwa ndugu jamani hata ufanyeje they dont want to move from the dependence level to the indipendent level. Asanteni kwa mawazo yenu no more miradi ya Pwagu na Pwaguzi, I will stick to the education ya watoto tu basi, maana hao ndio ndugu wa watoto wangu sitaki wakiwa wakubwa waje kuwa mzigo na wao kama mimi ndugu zangu walivyo.
  • Mdau USA

    Mdau USA

    20 September 2012 at 06:54 |
    Bora nitoe charity maana marafiki na ndugu wengine hawatosheki wala hawana shukurani lakini mtu usiemjua atakushukuru kwa kidogo ulichotoa.
  • Anonymous

    Anonymous

    20 September 2012 at 07:03 |
    mukeya likes tobirthdaydance get rich andletspartypopchampgnecheersdrinkbeer lolblowkiss
  • Anonymous

    Anonymous

    20 September 2012 at 07:05 |
    Can I be your friend LOL....Maana it will hard to be your friend when you are rich...no matter what I would do, it is going to look like I am kissing your ass..so the best thing I can do it try to be your friend now rather than later....LOL. I am serious girl. I am also very giving as well, but may be not so humble sometimes...Good luck with everything you are doing,the sky is the limit for you honey.
  • irene rouse

    irene rouse

    20 September 2012 at 07:14 |
    Hi Mange, i really dont know you, but i agree 100%.
  • maudodo

    maudodo

    20 September 2012 at 07:36 |
    mange you are so kind, na unapenda kila mtu awe na maendeleo ili ajikwamue na umaskini, but kuna watu hawasaidiki, unaweza kumsaidia kwa kumpa kiasi kidogo na kumweleza jinsi ya kukitumia ili aache kuwa tegemezi basi ye atafanya tofauti kesho anakuja kuomba tena khaaaaa... yani watu kama hao kuwasaidia ni ngumu sana.....Ila ni vizuri mtu ukiwa nacho kuwasaidia waso nacho, coz mkono utoao ndio upewao....!
  • maudodo

    maudodo

    20 September 2012 at 07:54 |
    mange nimeona mama(Dr. Mwele) katunukiwa tuzo mlete huku tumpongeze mama yetu, anajituma sana she deserves kwakweli...popchampgnecheers to her
  • RUKIA BINTI KASRI

    RUKIA BINTI KASRI

    20 September 2012 at 07:58 |
    heeee familia kula bata lazima,mm siku ya kuwa tajiri hata kile kiasi cha kuweza kumnunulia rafiki mafuta kwa gari yake kila mtu atajua looooo,jinsi ambavyo ntakua nawashwa kusaidia,siku yaja.
    • YOUSOU

      YOUSOU

      20 September 2012 at 19:15 |
      Hahahahahahaha nakupenda kweli Rukia binti kasri mchangamfu sana
      • Rukia Binti Kasri

        Rukia Binti Kasri

        21 September 2012 at 09:34 |
        Jamani Yousou asanteblowkiss mefurahi mmcheers
  • muke ya jaluo

    muke ya jaluo

    20 September 2012 at 08:16 |
    KWELIceo TUNAKUOMBEA UZIKAMATE SISI MASHOST TUFAHIDI INSHALLAH MUNGU NI MWEMA UTAZIPATA TU
  • Anonymous

    Anonymous

    20 September 2012 at 08:18 |
    Mange dear, sijui tumfanyeje huyu kondoo mweusi anaye jaribu kwa namna yeyote ile kukuharibia ndoa yako. Wanajitapa eti wametuma mauchafu kwa wakwe zako. Jamani, hivi binadamu unaweza kuwa mzuri wa sura ila mchafu wa roho hivyo? Sasa Mange akiachika wewe utaolewa na Lance? Angalia MUNGU asije kukupiga bonge la kibao. Nina imani hata siku tukikwambia utueleze kwanini uligombana na Mange mpaka ukamfungulia blog ya matusi huna sababu. Sasa kwanini usiendelee na maisha yako? muombe MUNGU na wewe atakupa mume wako, natamani nikutandike vibao na hivi ulivyo jirani yangu, sijui kama hata nitaweza kukusalimia tena. Jinga weeeee!!!!
    • Nai Nai

      Nai Nai

      20 September 2012 at 22:28 |
      Nyie waacheni wafanye watakavyo hao ibilisi, msiwalete humu kabisa, mwajua ngoma ikilia sana mwishoe inafanyaje? Sasa huu ni wakati wa hiyo ngoma kurindima maana i njiani kupasuka.

      Tena msiwe mnaleta humu habari zake kabisa wala musimuongelee. Jamani keep her away from us we dont want bad vibe humu ndani I begooo!

      Mange please dont post anything kuhusiana na huyo dada, please please naomba unisikilize mie, waswahili wanasema kamba hukatikia pembamba please stay away from her, dont post anything kutoka kwa wapenzi wako wala kutoka kwake, I mean anything, hata mtu akiandika kwa mafumbo dont post it please. Wewe from now on usimsemeshe, usimjibu, wala usifanye chochote just stay clean, kisha muachie Mungu afanye kazi yake.
      • Anonymous

        Anonymous

        21 September 2012 at 09:41 |
        myceo please sikiliza ushauri wa dada NAI NAI. tumwachie MUNGU ndie mwenye suluhisho la kila kitu
      • Muke Ya Albino

        Muke Ya Albino

        21 September 2012 at 13:15 |
        AMEN Nai NAIblowkiss
  • Isabell Arroyo

    Isabell Arroyo

    20 September 2012 at 08:52 |
    Mange me mbna celewi hzo votes jamani! Guess dt ws nat fair!!! Ebu pls go n re-read Competitant No. 7 & 16, yan wamezingatia vigezo na masharti yan wameeleza wanavyopenda na wacvyopenda kwko.. Bt hyo No.8 ambae ana more votes thn othrs me cdhani km amezingatia masharti japo I do agree kwmba ametiririka kishairi zaid! Othr thng naona km vile amebase kwny mipasho snaaaaa, k2 ambacho cdhani km ts a ryt thng... But hayo ni maoni na mtazamo wng2!!fan
  • lucky

    lucky

    20 September 2012 at 09:23 |
    MK, I love you so very much.... take my five.
    Inshaallah Mwenyenzi azidi kukuongezea ili usaidie hao uliowataja, mimi nikiwa mmoja wao, Amina.
  • Mange's fan

    Mange's fan

    20 September 2012 at 09:35 |
    Its true my dear even Mungu anabariki wanaosaidia wasiojiweza, Mungu atuzidishie nasi tuweze saidia wengine
  • sushi-puppet

    sushi-puppet

    20 September 2012 at 09:38 |
    KAMA NTAKUWA NIMEKOSEA SORRY BUT I FOUND THIS COMMENT SEHEMU FLAN THOUGHT U SHOULD KNOW HOW EVIL HUMANS ARE..
    (kokolikoooooooo hodi hodi magomeni kwa manyonyo watch out you are messing with a wrong whore bitch, kwiii kwiii kwiii wasema mashauzi yanataka pesa team minesota tunakwambia uchafuzi wa hewa hauitaji pesa bishosti tunadili na wakwezo Houston kwii kwii kwii tumechafua hewa mbayaaaaaa sikia hii mama mkwe tumeorder dildo catalog zimfikie home kwake babamkwe gay underwear catalogs shemeji yako cha kununa stripper catalog wifi yako T Stripper catalog kwiii kwii mbavu zangu jamani sipati picha catalogs zikianza kumiminika kaa mafuriko ya jangwani hizo sura za wazungu kwiii kwiii nakufaaa kicheko uchafuzi wa hewa muda wabonyeza kitufye kwishney nani kanuna leo wananchi mwasemaje na majirani nao? kwii kwii rahajeeee nifungulieni moet ninywe mieeeeeee te he te heeeee kwa msiojua dildo ni nyeti za plastic pata picha sasa mama mkwe anafunua catalog akutana na kila rangi za black, white kijani uwiiii uwiii)
    • Nai Nai

      Nai Nai

      20 September 2012 at 22:54 |
      Kwa hiyo hii ndio lawsuit waliokuwa wanasema wanaenda kufungua? Na bado watashuka chini zaidi ya hapo walipofikia. Next time usilete bad vibes humu, waacheni waadhirike huko huko kwao.
    • Anonymous

      Anonymous

      21 September 2012 at 01:46 |
      mmetuma salamu mmejibiwa kaaazi kweli kweli
      • Kijaruba

        Kijaruba

        21 September 2012 at 09:09 |
        Ishakuwa salaam zimetumwa kutokea huku? Au huku ndiko zilikoanzia? Kweli ubaya huonekana ulikoishia na siko ulikoanzia. Kwanza kama atayafanya hayo ndio atapprove kwa watu without doubt kuwa yeye ni Msazi kamili . Mtu mzima na akili yake timamu hawezi kufikiria hayo wala kuandika huo upuuzi, inaonyesha ni jinsi gani dunia imemuelemea. Maana kwa jinsi dunia ilivyo advanced a person can be easily tracked down, hata afanyeje there is no way whoever is gonna do this nonsense can avoid being traced. I didnt know kuwa bado watu wanafikiri kuwa waweza jificha popote duniani.

        Na kama kweli atayafanya haya basi Pole zake kwani KILA MTAKA NYINGI NASABA HUPATA MWINGI MSIBA!

        A point of advise arudi tu nyumba awe dada wa mujini atapata godfather atamtafutia kazi, atampangia nyumba prime area, atamfungulia na boutique na gari atamnunulia kuliko hivyo anavyojiabisha.
  • ivy

    ivy

    20 September 2012 at 10:09 |
    dats word sisy mange,being rich n watching others hanging with o beta life its realy bad,and even god doesnt give his smile for dat.
  • Daisy Daniel

    Daisy Daniel

    20 September 2012 at 10:17 |
    Your light mange matajiri wengi hawapendi kusaidia masiki wanataka kuona kila siku wewe mtu wa kuomba msaada hawajui km ukimsaidia masiki utamuinua na utegemezi.

    Im happy for u and i really like the way your.
    wakuache
  • Sally

    Sally

    20 September 2012 at 10:36 |
    Mpaka uwe na kiasi gani Ndio ujione now I'm rich?
    • Mshamba

      Mshamba

      20 September 2012 at 20:40 |
      Swali zuri kwa watu wengi sana. Kila mmoja anajibu lake.
  • NWA

    NWA

    20 September 2012 at 10:38 |
    Bitch Pliiiiiiiiiiiiiiz!
  • Anonymous

    Anonymous

    20 September 2012 at 11:22 |
    umeongea vyema mange, mtu kama umejaaliwa unatakiwa uwasaidie na wasio na kitu. Na Mwenyezi Mungu atakuzidishia zaidi na zaidi
  • anonymous

    anonymous

    20 September 2012 at 11:29 |
    you spoke my language Mange. GOD WILL BLESS YOU MORE AND MORE
  • Anonymous

    Anonymous

    20 September 2012 at 11:33 |
  • TIGHEST PUM PUM

    TIGHEST PUM PUM

    20 September 2012 at 11:36 |
    you have a good heart, you have some flaws but dont we all. people have worse characters than u, worse hearts evil minded but they forget all that when they are busy looking and judging others. Kudoz baby girl..
  • kirikuuIII

    kirikuuIII

    20 September 2012 at 11:41 |
    yaani binadamu walivyokuwa wabaya wanapenda wakuone ukienda kuomba kuomba msaada kila mara kwao lakini kama ingelikuwa kila mtu ana msaidia mtu wa karibu yake katika shida mbalimbali basi believe me dunia isingekuwa na watu wanaokufa kwa njaa au kuwa na watu wasiokuwa na elimu,,,
  • Mama Lisa

    Mama Lisa

    20 September 2012 at 12:32 |
    Darasa la dr. Mwele limekaa kichwani.....applause
  • Muke Ya Albino

    Muke Ya Albino

    20 September 2012 at 13:39 |
    Inshallah Mungu akujalie Utajiri unao-wish kuwa nao upate kunyanyua na wengine wengi.
  • Jarn

    Jarn

    20 September 2012 at 13:56 |
    i wan be your friend so u buy me those cl on my bday lol
  • Dee baibe

    Dee baibe

    20 September 2012 at 13:58 |
    i always have the same feeling , nikijaliwa kuwa hapooooooo , anyone who comes across me will kula bataaaaaaaa i don care if i know u ar not lazima ukule bata nooooomaaaaaaaa!
  • Anonymous

    Anonymous

    20 September 2012 at 14:16 |
    I wish ntakuwa yy one day
  • MANGEUKO JUU

    MANGEUKO JUU

    20 September 2012 at 14:33 |
    blowkisslickingukojuuwakuacheeducation

    YATOSHA MABANGO YANASEMA YOOTE
  • lolest

    lolest

    20 September 2012 at 14:38 |
    mbona kama sielewii,, No comment???? z it???waiting6969
  • nice urassa

    nice urassa

    20 September 2012 at 14:41 |
    i like manges blog jamani
  • lolest

    lolest

    20 September 2012 at 14:42 |
    Well Mange,, if i ever got dat rich...i guess ntasaidia sana watoto wasio na uwezo waende shule...educationpopchampgne kwanzacheers dat is the biggest investment...education
  • Anonymous

    Anonymous

    20 September 2012 at 15:44 |
    Mambo Mange, I've visited the other blog/site and saw s'thing wiered. They mentioned somethings abt your in-laws. Was a bit scared if what they've mentioned ni kweli. The blog inakuwa owned by a Tzn and those calling themselves mine..... have commented on that. Not sure if you've seen it, personally i did not like it.
  • Anonymous

    Anonymous

    20 September 2012 at 15:58 |
    Hupendi kuwa surrounded na un-happy people sawa but tht doesnt mean if u give them tonnes of money they will be happy...money unfortunately dsnt solve all the problems like unhappiness
  • kibonge

    kibonge

    20 September 2012 at 16:16 |
    nimemiss u turn jamani tangu last week sijaingia humu hadi nimepitwa na shindano la kujishindia viatu,nilikua nauguza mama ngu anaendelea vizuri sasa, pray for mama kibonge wana u turn wenzangu,
    • Mshamba

      Mshamba

      20 September 2012 at 20:44 |
      Tutamuombea. Pole sana kwa kuuguza!
      • kibonge

        kibonge

        21 September 2012 at 07:10 |
        THX WANGU,
      • Muke Ya Albino

        Muke Ya Albino

        21 September 2012 at 13:17 |
        Pole kwa kuuguza Kibonge, we will keep mama in our prayers.
        • kibonge

          kibonge

          21 September 2012 at 22:25 |
          AMINA MUKE YA ALBINO
    • Anonymous

      Anonymous

      21 September 2012 at 09:42 |
      pole dear, MUNGU amponye mama yetu.
  • mamdogo

    mamdogo

    20 September 2012 at 16:45 |
    Ningemjengea mamaangu na babaangu nyumba ya kuishi! maana pale na haya sijuwi maelninyo! presha inapanda presha inashuka, sijuwi watasalimia maskini ya mungu kwenye kile kijumba!NINGEHAKIKISHA familia yangu yote kila mtu anaishi maisha standard mwisho ningesaidia wasiojiweza!
  • Mama wa wili

    Mama wa wili

    20 September 2012 at 17:31 |
    You know what mange not every one has the same mind as you lol they some people are really rich
    and wachoyo kama nini paka unashagaa mbona Mungu anawazidishia bado Lakini kilakitu mungu ndio anapanga usiofu one day will be you, usinisahau jamani.blowkiss
  • MRS SOLIS

    MRS SOLIS

    20 September 2012 at 17:32 |
    batting eyelashesthumbs upthumbs upmoonwalker NOTHING TO SAY!!
  • Butterfly

    Butterfly

    20 September 2012 at 17:36 |
    Hapa bora nipite tu nisijefanya dhambi ya kutamani bure
  • MRS SOLIS

    MRS SOLIS

    20 September 2012 at 18:08 |
    IF I GOT SUCH MONEY I WOULD ALSO DO THE SAME LIKE YOU MANGE, HELP THE OTHERS..NIMESOMA KATIKA SHULE MOJA YENYE MOTO WA "MEN AND WOMEN FOR OTHERS" SO NINGESAIDIA JAMII KADIRI YA UWEZO WANGU, NINGEANZISHA MIRADI YA MAENDELEO PIA KUINUA NCHI YANGU SABABU NATAMANI SANA KUONA MABADILIKO KWENYE JAMII ZETU HASA VIJIJINI AMBAKO MAISHA BADO NI YA CHINI MNO. KWA KWELI NINGESHARE WITH OTHERS!!
  • RESPONSIBLE WOMAN

    RESPONSIBLE WOMAN

    20 September 2012 at 19:41 |
  • muke ya kenzoki

    muke ya kenzoki

    20 September 2012 at 20:37 |
    Mhh wewe unayetumia jina langu nitue plz!hizo cl zisiwatoe roho mpaka mkawa wezii wa majina ya watu !
  • Team MSHAMBA (Mshamba's #1 FAN)

    Team MSHAMBA (Mshamba's #1 FAN)

    20 September 2012 at 23:56 |
    newpostfreedom SWALI KWA WOTE HUMU NDANI.
    JE MNAFANYA/MMEFANYA NINI KUUTAFUTA HUO UTAJIRI? HAO KINA OPRAH HAWAKAI TUU WAKIOTA KUHSU UTAJIRI BALI WANAJITAHIDI KUUTAFUTA. HAWALALI MPAKA SAA MOJA ASUBUHI BALI WANAAMKA SAA KUMI ALFAJIRI. UKIWA TAJIRI UNAWAZA JINSI GANI UTAENDELEZA UTAJIRI SIO JINSI GANI UTAUMALIZA HUO UTAJIRI.

    MSHAMBA!!!!!hakunaga COMMENTS ZAKO ZINA MAKE WHOLE LOTS OF SENSEsonya

    KAENI CHINI MTAFAKARIJINSI YA KUUPATA HUO UTAJIRI NA SIO KWA MDOMO. JINSI YA KUSAIDIA NDUGU JAMAA NA MARAFIKI, MSHAMBA KESHA WAELIMISHA HUKO JUU KWENYE POST YAKE.
    • Mshamba

      Mshamba

      21 September 2012 at 04:54 |
      Thank you!blowkissblowkissblowkiss
    • Mshamba

      Mshamba

      21 September 2012 at 05:53 |
      I agree with you completely. Lazima uwe na mipango na ufanye juhudi za kila aina kuhangaika na kuendeleza kipato. Ni jitihada za kila hali na kutokubali kushindwa ndiko kunafanya wengi wasonge mbele. Sisi huku bongo mtu akijaribu kidogo tu akashindwa au akapoteza hela kidogo tu anaacha na kuikimbia biashara badala ya kuangalia ni wapi mtu anakosea na kuboresha mapungufu ambayo yapo na kama ni makubwa sana ina maana kuwa hakuangalia vizuri vigezo vyote vya hiyo biashara kabla hajaianza. Kingine watu wanataka pesa kubwa mara moja ghafla. Biashara haziendi hivyo lazima kwanza pesa ikutoke kama mtaji wa kutengeneza biashara yako (capital) na hii hutofautiana kulingana na biashara yenyewe.
    • Anonymous

      Anonymous

      21 September 2012 at 14:23 |
      me hapa nina mipango kibao..I know one day yes na God knows ma plans for ma people jmn.wl make them smile one day.
  • kuntuafro1

    kuntuafro1

    21 September 2012 at 05:21 |
    Ni vizuri kusaidia watu lakini tatizo bongo mawhitch kibao ukiwasaidia wanakuroga. Africa maendeleo duni. Unawasaidia ili wajikwamue wanaona unaringa na vihela vyako. Labda ukoo wako uwe kama kina MAREALLE UKOO MZIMA MATAJIRI lakini hizo koo zetu hizo lazima WAKUUWE.
    • Nai Nai

      Nai Nai

      21 September 2012 at 08:11 |
      Usiogope kuwhitch kutokana na kumsaidia mtu, kwani ule msaada unaoutoa ndio kinga ya uchawi wao akienda kufanya huko atadhurika mwenyewe wakati wewe unazidi kubarikiwa. Unachotakiwa kufanya ukitoa huo msaada unasema nimetoa hii kwa ajili ya muumba wangu, basi unaishia zako usiyafuatilie ya nyuma labda mwenyewe arudi kuja kukwambia kakwama.
  • Anonymous

    Anonymous

    21 September 2012 at 11:00 |
    Dear Dada Mshamba,
    My email is wendyalex96@yahoo.com, naomba unitafute plz i have tried to look for your email in the previous posts but sijaona. its very important mpenzi wangu.

    Thanks,
    Wendy.
    • Mshamba

      Mshamba

      21 September 2012 at 22:38 |
      Tayari Wendy!
  • bree@pretender

    bree@pretender

    22 September 2012 at 17:15 |
    ningesaidia wazee na vikongwe wenye shida na wagojwa wasio na ndugu mahosipitalini ningepika chakula nile na wenyenjaa wanaoishi kwa mlo mmoja kwa siku i mean one dola per day ningesaidia watoto wachanga waliopoteza wazazi and family
  • Mshamba

    Mshamba

    21 September 2012 at 22:16 |
    Muke ya Albino,thumbs up
  • sa

    sa

    23 September 2012 at 03:44 |
    Ubarikiwe pia dear