06July

WATOTO WANAHITAJI MSAADA.....

Dear Dada Mange
Hivi karibuni nilienda kumtembelea mama yangu mkubwa aishie mbezi makabe,huyu mama yangu ni mwalimu,kwa bahati nzuri nilipata bahati ya kutembelea shule anayofundisha inayoitwa makamba,kusema kweli hii shule wanafunzi wana hali ngumu sana,katika darasa moja kuna dawati moja tu na wanafunzi wengine wote wanakaa chini.Niliumia sana,Nikajaribu kuongea na mwalimu mkuu akasema ni kweli hali ni mbaya sana,wanamatatizo mengi lakin kubwa linalowaumiza zaidi ni madawati kwan utakuta katika darasa moja kuna dawati moja tu.
Dada Mange tunawezaje kuwasaidia hawa wanafunzi?
Hii ni picha ya darasa niliopiga hapo shuleni.
Dada naomba uwasiliane na mimi jumatatu, ntakupa chochote kidogo nilichonacho. ungeweka na number yako ya simu ili na wengine watakaopenda kusaidia wakupigie simu. Ila naomba urudi kutueleza msaada walioupata hawa watoto.....

MANGE KIMAMBI

Comments (31)

  • muddy washington

    muddy washington

    06 July 2012 at 04:20 |
    wadau tuoneshe ushirikiano wa kutoa comments kwenye hili kama tulivyoonyesha kwenye issue ya dada muogopa kutolewa bikra.Lakini pia tusiishie kuchangia comments bali pia kuona jinsi gani tunaweza kusaidia,hivyo nategemea comments zifunike issue ya bikra na ziwe constructive.

    asanteni
  • Anonymous

    Anonymous

    06 July 2012 at 06:55 |
    Fuck you mange
  • Anonymous

    Anonymous

    06 July 2012 at 07:17 |
    Maisha Bora Kwa Kila Mtanzania!
  • Anonymous

    Anonymous

    06 July 2012 at 08:55 |
    Mange be careful,kunamatapeli usiombe.Chakufanya hapa ni bora ulianzishe mwenyewe,amua kuchangisha wewe mwenyewe na ukaziwakilishe wewe mwenyewe,usimpe mtu hela bila kumjua vizuri,na ningumu sisi kumpa mtu hela tusiomjua sisi tunakujua wewe tu.Please jitolee kwenye hilo tukuchangie maana watoto kweli wanahitaji msaada.
  • mama peace

    mama peace

    06 July 2012 at 09:02 |
    Hi Mange,tafadhali naomba umsihi huyo dada aweke contact zake ili tuweze kuchangia zaidi,maana ni vibaya kuona tunaweza kuspend zaidi ya elf 50 na kushindwa changia watoto wetu dawati hata moja
  • Anchiwela

    Anchiwela

    06 July 2012 at 09:44 |
    Tanzania nchi yangu nakupenda lakini mhhh kazi bado nikubwa hivi watu wanajisikiaje kujilimbikia mimali while this children suffer in such bad studying conditions na hapo ni dar huko vijijini inakuwaje, lord have mercy jamani
  • Anonymous

    Anonymous

    06 July 2012 at 09:49 |
    UNTUZINGUA NA KUTAFUTA UMAARUFU TU.
    KISA ANAFUNDISHA MAMAKO NDO UNAONA WANATESEKA?
  • c's mum!

    c's mum!

    06 July 2012 at 10:19 |
    KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI!!!!
  • koku

    koku

    06 July 2012 at 11:32 |
    napita jamaniI don't know
  • anonymous

    anonymous

    06 July 2012 at 12:24 |
    i feel so sorry jamani kwa hao watoto, ila shule pia huwa inajengwa na walimu sio serikali peke yake,mimi nilisoma shule mkoa ilikuwa moya, tulikuwa tunachanga hela kidogo tena kama mia hivi kwa wiki, then tulikuwa tuna miradi ya shule midogo, mfano shule ilikuwa imapika uji, chai na vitafunwa kwa hiyo tunanunua hapo harafu faida ilikuwa inawekwa kujengea shule, na mwalimu mkuu alikuwa anafanya harambee, na siku ya graduation anaelezea faida za miradi ya shule, na amefanyia nini, sasa walimu wengine wakiwekwa sehemu basi wanabweteka tu hakuna wanalofanya. Nendeni mkaone shule ya msingi uhuru mchanganyiko na yule mama anavyoipenda shule yake, aibu yake mwalimu mkuu na si mfatiliaji. mbona kuna shule vijijini zina madawati? nawashauri walimu wasibweteke jamani, waijenge shule wenyewe, uongozi ni kitu muhimu sana, nilisoma shule za masister pia ada ndogo ilikuwa kijijini lakini pesa inayopatikana walikuwa wanaitumia vizuri.
    huo ndio mchango wangu ila naomba na walimu waelimishwe.
  • Anonymous

    Anonymous

    06 July 2012 at 14:03 |
    Its sad and touching. Shule iliyo karibu na waendesha mapajero.

    Kumtumia hela tu kienyeji sio busara. Iwe a bit organised kwamba zikusanywe na kukabidhiwa mwalim mkuu au iwekwe order ya madawati na kupeleka madawati moja kwa moja.

    Ushauri tu jamani.
  • koku

    koku

    06 July 2012 at 14:34 |
    ushauri wangu ni kuwa, tafadhali uliyeleta mada weka bei ya dawati ni shs ngapi. halafu mi nitamtuma mtu wangu wa karibu kununua na kulipeleka. haya mambo ya michango yanamuharibia mange reputation yake..kiss
    • Anonymous

      Anonymous

      09 July 2012 at 06:00 |
      Hata akiweka utachanga wewe??embu acha kusumbua watu,we si mchangaji zaidi ya michango ya comment tu
  • KUNTU

    KUNTU

    06 July 2012 at 20:53 |
    Hii ni aibu,itabidi niwachangie kununua madawati, sikujua kama ile shule ya Makamba wanakaa chini,iko karibu na kiwanja changu.Kumbe ata kule nako watoto wanakaa chini???? Yusuph Makamba ndio alikua Mgeni rasmi katika ufunguzi wa hii shule didn't know that hawana Madawati masikini.
  • Anonymous

    Anonymous

    06 July 2012 at 21:57 |
    msaada unaombwaje kienyeji hivi?tuna uhakika gani matumizi yatakua sahihi?tuta ku-hold vipi accountable?kajipange wewe acha sanaa!
  • Oscar Mashauri

    Oscar Mashauri

    06 July 2012 at 22:13 |
  • Mwananchi

    Mwananchi

    06 July 2012 at 22:20 |
    Mange & co sikilizeni acheni papala kuna shule huko bush wanasomea chini ya mibuyu and no one anajali, cha kufanye ni kuwaaumbua hao wanaoweka ma trillion uswizi wazirudishe zijenge nchi, I'm just mwananchi na not interested in politics. Ni jukumu la serikali mtachangishana wee but u will never get rid of these problems but vioongozi wa nchi wakijipanga nchi yetu ni tajiri na inawezekana. Acheni kupoteza muda na blabla za kutwanga maji kwenye kinu, karne ya sayansi na technolojia, miaka 50 ya uhuru is so shameful to see that we still living in stone age era
  • mangekimambi

    mangekimambi

    06 July 2012 at 22:59 |
  • uturnaddict

    uturnaddict

    07 July 2012 at 10:22 |
    Mange usimpe huyo dada pesa watu hawaamini siku hiz!

    Kanunue madawtu unayoweza peleka kwani hupajui?

    We waambie watu wachangie halaf uangukiwe na jumba bovu
  • uturnaddict

    uturnaddict

    07 July 2012 at 10:23 |
    Halafu mbona nyumba ya watoto yatima hujatuonesha tena?
  • nainai2

    nainai2

    07 July 2012 at 15:14 |
    Jamani tufike mahala tuangalie njia mbadala ya kisolve hii ishu ya madawati.

    1. Kwanza kutengeneza madawati ya mbao ni uharibifu wa mazingira, jinsi tunavyozaa watoto wengi na population inavyozidi kuongezeka lazima tukate miti ya kutengeneza madawati zaidi kwa hiyo madawati ya mbao sio sustainable solution.

    2. Madawati ya mbao yanaharibika haraka ukizingatia aina ya mbao inayotumika kutengenezea na magumashi ya mafundi wetu, kwa hiyo unaweza kujaza darasa zima madawati by next year hakuna kitu.

    3. Hatuna utamaduni wa maintanance, madawati yanayoharibika badala ya shule kuwa na karakana za maintanance na repair, na kama sio shule basi ofisi ya kata; madawati yanayoharibika yanaishia kufanywa kuni za kuchemshia maji ya kuoga kwenye nyumba zilizo karibu, au kuni za kukaangia mihogo.

    Tufanyeje?

    Umefika wakati sasa wa kutafuta njia mbadala ya kuwapatia watoto vifaa vya darasani. Nafikiri tutumie aina fulani ya viti vya plastiki ambavyo ni vidogo na ni size ya watoto kama wanavyofanya nchi zilizoendelea. Viti vikiwa vikubwa vitaishia kwenye BAR, PUB, Glosari sijui na vilabu vya pombe au kwenye vijihoteli vyetu au kwa mama ntilie. Lakini vile size ndogo hawawezi kuvitumia kwa matumizi mengine.

    Kuhusu kuandika, tuige wasouth Afrika wanavyotengeneza zile hand desk za plastic ambazo wanatumia kupunguza uhaba wa madawati.

    Shule nyingine za majuu zimewekwa kapeti tu watoto wakiingia darasani wanavua viatu wanakaa zao chini pasafi mwalimu anaendelea na somo hasa pale wanapochanganya madarasa na kuwafundisha watoto wengi kwa pamoja. Ila ikifika wakati wa kuandika ndio kwenye madawati. Idea ya kuweka kapeti darasa zima inafaa tu pale ambako kuna usafi wa hali ya juu na sio kwetu, lakini kwa mfano kwenye hilo darasa pangetandikwa kapeti kwa muda watoto wakasoma wakati uvumbuzi wa kudumu unaafutwa ingekuwa poa tu.

    Nai Nai


    pili ni ra
    • kuntuafro1

      kuntuafro1

      08 July 2012 at 23:12 |
      I like your idea NaiNai,Sisi kama wana uturn tunge come up nayo instead of kununua madawati tungenunua hivyo viti na videsk vyake,alafu hizo Stackable School Chair aint that expensive, wanafunzi wangekaa vizuri kwa nafasi bila kubanana.I KNOW UTURN TUNAWEZA.
  • mimi

    mimi

    07 July 2012 at 17:59 |
    elimu ya bongo hiyoooo! mange wewe umetoa nini kwanza?
  • Anonymous

    Anonymous

    07 July 2012 at 20:41 |
    Why not appear
  • WA MIGO MIGO

    WA MIGO MIGO

    07 July 2012 at 22:26 |
    chezea mange wewe! utalala hounot worthynot worthy
  • Anonymous

    Anonymous

    08 July 2012 at 22:45 |
    kila mmoja wetu akitengenezesha dawati moja pale kwa fundi mangungo then akalipakia kwenye RAV4 yake na kulisubmit hapo shuleni kazi itakua rahisi sana kuliko tunavyotarajia,na tunazishe kampeni hiyo ya kila mtu kwa mwaka ajiwekee mkakati wa kutengenezesha dawati moja na kuligawa kwenye shule hizi za lowassa(kata)
  • Anonymous

    Anonymous

    09 July 2012 at 09:47 |
    Namba ya mtoa mada ni 0767552287 lakini pia kwa wale walioguswa na wanaotaka kutoa michango yao wanaweza kuituma kwa mkuu wa shule anaitwa Mr.Joseph
    Kalomba na namba yake ya sim ni0713309366 na msaidizi wake ni zania
    senkondo namba yake ni 0655852077, kwa wale
    wanaotaka kupeleka hayo madawati wanaweza either kuyafikisha shuleni au
    kuwasiliana na hizo namba za walimu hapo juu watayapokea kwa mikono miwili.
    Kuhusu bei za madawati ni kati ya 75000-80000 kutegemea na aina ya dawati.Ila naamini kwa wale watakaotembelea hapo shule mwalimu mkuu na msaidizi wake wanaweza kutoa maelezo zaidi kuhusu haya madawati.
  • Aisha

    Aisha

    09 July 2012 at 09:55 |
    Namba ya mtoa mada ni 0767552287,lakini kwa wale walioguswa zaidi wanaweza kutuma michango yao kwa mkuu wa shule Mr.Joseph
    Kalomba na namba yake ya sim ni0713309366 na msaidizi wake ni zania
    senkondo namba yake ni 0655852077,kwa wale
    wanaotaka kupeleka hayo madawati wanaweza either kuyafikisha shuleni au
    kuwasiliana na hizo namba za walimu hapo juu watayapokea kwa mikono
    miwili.
    Mungu awabariki sana
  • Mdigo

    Mdigo

    09 July 2012 at 11:11 |
  • Anonymous

    Anonymous

    10 July 2012 at 13:27 |
    vitu vyako ni vizuri san dada mange