|
JAMANI NISHAURINI JUU YA HUYU MUME WA MTU.... |
|
Written by Mange
|
|
Monday, 15 March 2010 19:26 |
|
Hi Mange
mi nilikuwa naomba ushauri juu ya huyu mume wa mtu.Huyu mkaka ni kwamba alikuwa anaishi na mkewe huko Mwanza sasa akahama kikazi akaja hapa Dar akamwacha mkewe huko Mwanza anaendela na kazi alipofikisha karibia miezi sita akamwambia mkewe aje kuishi nae hapa mkewe akakataa kabisa sasa yule kaka akaendelea kuishi hapa akawa anaenda au mkewe anakuja wakti wa likizo kumbuka hapo wana mtoto mmoja tu.Sasa huku kazini nikawa nimekutana nae mie na kwa mara ya kwanza sikujua kama ameoa kabisa ila baadae aliniambia na akasema ananipenda sana basi tumeendelea na uhusiano mpaka hivi sasa. Ila sasa yule mkewe kumbe akawa kuna mtu anatoka nae kule Mwanza na mapenzi mazito kiasi kwamba kila mtu mpaka ndugu wa mwanaume wakajua na wakamshauri aachane nae maana anatia aibu sana huko Mwanza basi mkaka akaona hapa ndiyo safi akaniambia kuwa anataka kunioa mie na yuko serious mpaka kaanza kunitambulisha kwa ndugu zake na mkewe kashamwambia hataki.
Sasa nie sijajielewa nikubali hii ndoa au nikatae maana naona inanichanganya sana.
Naomba ushauri kwenye hili na kumbuka mwanaume nampenda pia
Mdau,Martina
|