|
Sijui pa kuanzia, but for the past few month I have struggling with excess saliva on and off…eewww….
Nimejaribu ku-google mpaka nimechoka bado sijapata dawa yake. Hakuna kitu nachokichukia kwenye maisha yangu sasa hivi kama hichi kitu cha kutema tema mate. Its so disgusting, na kuna wengine huwa wananikata jicho kama wanatamani kunitukana wanashindwa ila nashindwa kujicontrol sio makusudi na kuna siku kuna baba aliniangalia vibaya kidogo nimtukane…hahaha…
Basi nimefikia sehemu kwamba nikiona siku hiyo nashindwa kabisa kujizuia kutema tema mate basi najifungia ndani siendi kwa mtu wala nini kwa vile najua kuna wengine nawakwaza.
Masikini shoga zangu naona sasa wamezoea tu mpaka hawaoni tena kinyaa, ila inanisaidia kwamba marafiki zangu wengi na wao pia ni wajawazito kwa sasa so they are being understanding as a matter of fact kuna mmoja wa rafiki zangu nayeye na hili tatizo kama langu, that has been comforting to me in a way...
Anyways, swali langu wadau hivi kuna dawa ya kuweza kunisaidia niache kabisa kutema tema mate kama kibibi kinacholamba ugolo? Au kama wale wasomali wanaokula mirungi? LOL
Swali lingine ni hili, kuna watu nilikuwa naongea nao kuhusu huki swala la kutema mate ovyo mmoja wao (mwanamke) akasema wanawake wa kiafrica tukiwa na mimba tunajiendekeza tu, mara kula udongo, mara kutema tema mate ovyo, mbona wazungu hawatemi mate wakiwa wajawazito?
Mdau, hivi ni kweli wanawake wa kizungu hawatemi temi mate wakiwa na mimba?nime-googgle na nikaona kwamba kuna wanawake wengi kwenye internet wanaongea swala zima la kutema mate na nimehisi ni wazungu. Wewe unalionaje hili swala?
I know it’s a disgusting topic to discuss but nielimisheni jamani na pia nisaidieni dawa ya kuachana na haya mateso….USISTA DUU WOTE UMENIISHA AISEE…HELLLLPPPP

|