|
Dear Mange, ( naomba mail yangu usiitoe hadharani pls) Naomba ushauri wako na pia kwa wasomaji nisaidieni nimechanganyikiwa mimi naishi China ,nilikutana na jamaa mtanzania china alikuja kwa shangazi yake anae ishi China jamaa anasoma ( Marekani ) tulipendana sana na uhusiano wetu hivi sasa ni mwaka moja , na kwakuwa anasoma marekani huwa anakuja china kuniona mara mojamoja. na akiwa marekani huwa ananipigia simu kila siku, tunawasiliana vizuri tuu, mara ghafra akaanza kubadirika, tukawa tunagombana kila siku ikawa ni kero, sasa basi, jamaa alinificha kuwa ana demu mwingine mzambia ambae alikuwa demu wake wa zamani wakati wanasoma collage, na amekaa nae all most miaka 2. mimi niligundua kwa kupitia hizi site za kutafuta urafiki,( internet) jamaa yangu alikuwa huko na huyo demu pia wanawasiliana kwenye hio site , ni mapenzi matupu, na kutongozana humohumo na kukumbushana , kila kitu kiko open any body can see, na huwa wanaandikiana kila siku nilivyoona ilibidi nimuulize kulikoni, Alishtuka kwanza, hakutegemea kuwa naweza kujua, akanijibu alikuwa demu wake wa zamani, na alikuwa anampenda na hawakugombana kwahio sio mbaya kuwasiliana ila maneno yasiniumize kwani ananipenda mimi, ndio chaguo lake,, nahisi kama wanapigiana simu ila sijawahi kumkamata, mbaya zaidi ukoo wa huyo demu wake wa zamani jamaa anawafahamu wote na pia demu ana 100% kuwa jamaa anampenda( kwa kuangalia maongezi yao.) Sasa wadau kila siku ananiambia ananipenda, mimi, sielewi kama ni kweli au laa, nikiongea na jamaa kuhusu huyo demu anajifanya hakumbuki na haelewi na hataki kuongelea, anasema kuwa mimi ndio demu wake, nisaidieni mawazo jamanii jamaa simwelewi hata sijui nimfanye nini?
Sarah
|