|
Guys,
Nimefikiria nimeona kwamba ni bora siku hiyo ya shughuli tuende watu wachache, meaning tusizidi 50. Ili tusitumie pesa nyingi kwa ajili ya hiyo lunch ili tutumie pesa nyingi zaidi kutoa misaada.
Nimeona bora event iwe ya kawaida sana,tena sana, meaning kusiwe na makuu kabisa, ili msaada uwe mkubwa zaidi.
Wote tutakaokwenda tutavaa T-shirt za red, ambazo zimetolewa kama mchango na rafiki yangu kipenzi Joseline.
Tumetengeneza tshirt kwa size tofauti , small, medium & Large.
Kama ungependa kwenda kwenye hii event pls nitumie email humu
This e-mail address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it
.
Jamani naomba wale waliotoa michango tu ndo wajitokeze kwenda. Sababu sidhani kama itakuwa na maana kama watakwenda wengi ambao hawakuchanga chochote nikawaacha waliochanga.
Pia nimeona tusiende na watoto wetu, sababu tukienda na watoto wetu tutakuwa busy zaidi na wanetu na sio wale watoto yatima ambapo sasa tutakuwa hatujafanya cha maana sababu point nzima ni kuwapa mapenzi wale watoto. Mie najijua Kenzo wangu nikienda nae sehemu ambayo hajui watu ananing’ang’ania nimbebe.
Event itakuwa siku ya jumapili Feb 12.

|