|
KUELEKEA EVENT YETU YA VALENTINE'S DAY..... |
|
Written by Mange
|
|
Tuesday, 31 January 2012 21:21 |
|

Leo nilienda tena Kurasini National orphanage centre.
Lengo langu leo lilikuwa ni kuongea na management ili tupange vizuri
mlolongo mzima wa event.
Alhamdulillah, everything went well...

Then nikaenda kuwaona wale watoto wadogo, wakubwa bado
walikuwa shule...
this is them taking their afternoon nap...
yes ,they nap kwenye mkeka....sakafu inavyoumiza sasa
ila usiku wanalala kwenye dorm zao...

Chatting with the kids...i love this little girl...she is super cute, her name is
Asha, jina la marehemu mama yangu hilo....


Hanging out with the kids...

nilijairbu kuuliza kwanini watoto wanatembea bila viatu au hata
kandambili. nikaambiwa wamepoteza...
sasa wakikanyaga miba inakuwaje jamani...
one of the things i plan to buy ni kandambili....

Also i asked kwanini watoto ni wachafu, nguo ni chafu,
nkaambiwa hawana nguo za kutosha,
so kwa wale ambao hamna uwezo wa kutuchangia cash
tafadhali kama una nguo za watoto used naomba unipe....

nikiwa na watoto wachache kati ya watoto 117 wanaolelewa hapa...
wengine ni wakubwa zaidi niliambiwa bado wapo shule...


they are such happy souls....

Huyu binti alinisikitisha jinsi alivyoharibika ngozi....


ngozi ya mtoto...

Nikimuonyesha mlezi wao jinsi mtoto alivyoharibika ngozi
na nikimuuliza wanampaka dawa gani, au kama keshafika kwa daktari.
nikajibiwa mtoto ni mwathirika wa HIV.
nikamwambia hilo sio jibu dada hata kama ni mwathirika,
still anatakiwa awe anatumia dawa kwa ajili ya hii.....
i felt really bad....

Nikicheka na watoto....

last time nilivyokwenda wakati naondoka niliwaambia watoto nawanunulia soda
na biskuti ,basi nikamwachia kaka mmoja pesa,huyo kaka ndo alienipokea siku hiyo.
basi na leo wakati naondoka nikawaambia tena watoto nitawanunua soda na biscuit,
kitoto kimoja kina kama miaka 5 hivi kilinishushuaje sasa,
akasema, we dada miyeyusho, hata mara ya mwisho ulisema utatununulia soda hukununua
uwiiii, kabla sijajibu nilianza kucheka kwamba,
try to imagine katoto kadogo kanasema neno 'miyeyusho'
vitoto vina maneno hivi...
DUh ,i felt really bad kwa kweli, so nikawauliza wote kwa pamoja
mara ya mwisho nilivyoondoka hamkupewa soda au juice au biskuit
wakasema hapana hawakupewa.
i was just like DUH...
So, nikasema leo siondoki hadi nivione vimeletwa

nilikalishwa 1hr eti juice na biscuit zimefatwa dukani.
ila nilikaaaaaa, hadi vikaletwa nikawaacha wanakula ndo nikasepa zangu.
kwa kweli im disappointed jamani, sijui cha kufanya na nchi hii.
sijui ni huu umaskini umezidi hadi mtu anaweza kuwacheat watoto kama hawa
hela ndogo tu ya soda na biskuti???
Ila lesson learnt, hakuna kuacha cash, hata iweje,

Nikimfungulia mtoto juice...
yani kwetu sie juice na biscuit ni kitu kidogo sana, ila ungeona jinsi watoto
walivyoruka ruka baada ya kuona juice na jinsi walivyoniambia ahsante.

HOW DO WE CHANGE THINGS IN THIS COUNTRY???
HOW DO WE MAKE SURE MISAADA INAWAFIKIA WALENGWA???
Naomba muendelee kuchanga
Western union : Mange Kimambi Lowrey – Tanzania
MPESA: 0769 781315
|