|
Dear Mange,
Nina swali ambalo linahusu maisha ya kawaida , mi nina umri wa miaka 28, namshukuru Mungu nimesoma kiasi siwezi kusema nimesoma saaana , nina degree moja tu, na diploma mbili, Mange sio kwamba nataka kujishaua au vipi, nataka nikupe msing wa swali langu,
Ninafanya Kazi at least najikimu katika maisha na naweza kusaidia wazazi wangu kidogo na ndugu japokuwa sio sana.
Mange nimekuwa nikipata mawazo sana hivi karibuni, Tangu nikiwa mdogo nimekuwa nikimuomba Mungu niishampata mwenzangu nndo tupange Mipango ya watoto na kuwa na familia kubwa vyovyote vile tutakavyotaka,
Lakini kitendo cha mimi kuwa sijaolewa hadi sasa, naonekana kama nimechelewa sana na uwezekano wa kkuja kuolewa tena ni mdogo sana,
Nimekuwa nikipata maswali si kutoka kwa wazazi tu hata watu wa nje , kama sijaolewa kwa nini sina mtoto mpaka umri huu?
Mange hayo maswali yamekuwa yakinitatiza kiasi kwamba naona kama maamuzi yangu labda si sahihi,
Sasa swali langu ni hili je umri sahihi wa mwanamke kuolewa ni upi? na kama mpaka umri huu sijajua nitaolewa na nani ni kosa ni matumaini wana u-turn mtachnagia na si kutukana Email yangu kapuni please
|