|
Mwanamke umbea babu,halo halo.
Wanawake wenzangu kila siku mnaambiwa msiwe mnatembea na waume za watu hamsikii sasa labda leo mtajifunza kwa yaliyompata huyu bibie anaejidai ni superstar mji huu,
Basi huyu demu aliekuwa akiishi marekani ila alirudishwa kwa deportation mwaka jana (natamani kuweka jina ila nahisi mama uturn hatoweka article nikiweka jina lake,ila jina lake linaanza na R) alikuwa anatembea na mume wa mtu ,sasa badala hata awe na adabu au heshima kwa mkewe dada akawa kazi kumtukana huyo mke kwa meseji na kumwambia mumewe hatorudi tena kwamba yeye keshamshika.
Basi siku ya tarehe 10 may 2010 huyo dada alipotea ghafla baada ya kutekwa na mijaune minne yenye misuli, mijanaume hiyo ilitumwa na mke wa huyo jamaa aliekuwa anakula nae uroda,unaambiwa walimfanyia vitu vyote vichafu unavyoweza kufikiria wewe na pia walimpiga picha wakati wakimfanyia hivyo vitendo,
Baada ya hapo wakamtupa pembeni mwa barabara akaokotwa na mapolisi na kupelekwa hospitali,
Tena siku hiyo nakumbuka watu tulikuwa tunajirusha kwenye kiwanja kimoja hapa dar habari zilipoanza kusambaa kwenye kiwanja hicho kwamba R kafariki dunia wengine walianza na kulia wakidhani mdada kafariki kumbe habari zilifika vibaya alikuwa amelazwa hospital akiwa na hali mbaya sana.watu walipokwenda kumuona hospitali akawa anajidai kachanyanyikiwa hakumbuki kafanywa nini au hao watu walimpeleka wapi huku alikata kutoka hospitali siku hiyo hiyo akiogopa waandishi wa habari watafika hospitali.
Inasemekana huyu dada sasa hivi kaacha tabia yake ya story ya uongo ungo na kutembea na waume za watu, tena huyo mama aliemfanyizia amemwambia akimsogelea mume wake tu basi picha zitakwenda kwenye magazeti
Sasa nyinyi mliobaki na tabia hiyo jiangalieni sasa,watu tunawapenda waume zetu sasa endeleeni kujileta tutawatoa roho mwaka huu.
|