Who's Online
We have 271 guests online
Total number of Visitors
mod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_counter
mod_vvisit_counterToday7118
mod_vvisit_counterYesterday8768
mod_vvisit_counterThis week7120
mod_vvisit_counterLast week82441
mod_vvisit_counterThis month54192
mod_vvisit_counterLast month319970
mod_vvisit_counterTotal No. since we started4933759
Login



ETI ZANZIBAR KUWA NCHI KUANZIA OCTOBER????? NYERERE MUST BE TURNING IN HIS GRAVE!!! MAONI????
Written by Mange   
Wednesday, 11 August 2010 20:06

 

SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) inafanya marekebisho ya katiba ya mwaka 1984, ambayo yanaipa Zanzibar hadhi kamili kama nchi ndani ya Jamhuri ya Muungano.

Marekebisho hayo ya katiba yanatarajiwa kuwasilishwa katika kikao cha Baraza la Wawakilishi kinachoanza leo Zanzibar, ambapo pia yataruhusu kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa baada ya uchaguzi wa Oktoba mwaka huu.

Kwa mujibu wa rasimu ya marekebisho ya katiba hiyo, sura ya kwanza ibara ya kwanza iliyokuwa ikisomeka, Zanzibar ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imefutwa chini ya marekebisho hayo.

Rasimu hiyo ambayo itawasilishwa na Mwanasheria Mkuu, Idd Pandu Hassan, inapendekeza kifungu hicho sasa kisomeke ‘Zanzibar ni nchi ambayo eneo la mipaka yake ni eneo lote la visiwa vya Unguja na Pemba pamoja na visiwa vidogo vilivyoizunguuka na bahari yake, ambayo kabla ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar iliitwa Jamhuri ya watu wa Zanzibar’.

Aidha, marekebisho hayo ya katiba yamegusa kifungu cha pili na kueleza kuwa Zanzibar ni miongoni mwa nchi mbili zinazounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Marekebisho hayo pia yamegusa mamlaka ya rais katika kuigawa Zanzibar katika mikoa, wilaya na maeneo mengineyo kwa kufuata utaratibu uliowekwa na sheria iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi.

Kabla ya marekebisho hayo kifungu cha pili cha Katiba ya Zanzibar kilikuwa kikisomeka ‘kwa ajili ya utekelezaji bora wa shughuli za serikali, Rais wa Jamhuri ya Muungano akishauriana na rais anaweza kuigawa Zanzibar katika mikoa, wilaya na maeneo mengineyo kwa kufuata utaratibu uliowekwa’.

 

Kwa habari zaidi ingia humu

Comments
Add New Search
Anonymous   |2010-08-11 16:24:24
Sawa tu coz it doesn't make sense.kama sio nchi sasa kwanini kuna raisi wa
Zanzibar si angekuwa JK tu.
Nyerere kamariza wakati wake awezi kuturn in his
grave .
Wache tu wawe na nchi yao na raisi wao sema wakifanikiwa basi itakuwa
UARABUNI ya Africa.
Anonymous   |2010-08-11 19:57:26
WAACHE WAENDE ZAO......WANAONA WA-BARA TUNAFAIDI SANA
Anonymous   |2010-08-12 04:52:21
tutatakuwa tunagongewa visa kama zamani? hicho kisiwa kingebaki hivyo kilivyo
ati nchi, miundo mbinu sifuri kila la heri nchi ya zenji
Anonymous   |2010-08-12 05:14:46
Mange hiyo Zanzibar ni Nchi kama zilivyo nchi nyingine...Yaani mpaka ikaitwa
UNITED OF TANZANIA...Inamaana kuna muungano wa vitu 2....Nikimaanisha nchi mbili
Tanganyika na Zanzibar.....Na kiukweli ukiwa nje ya Tanzania si vizuri na wala
haikubaliki kujitambulisha au kusema mimi natoka nchi ya
zanzibar/tanganyika...KINACHOJULIKANA ULIMWENGU MZIMA NA KWENYE RAMANI NI
TANZANIA...

Tatizo hapa kuna kujikweza watanganyika tumeungana na watu
wabinafsi sana yaani waznz ni wabinafsi na watu wa kujikweza, wabishi na jeuri
ni wagumu pia kuelewa....Wanachotaka wao kwamba Zanzibar itambulike nchi hata
ukiwa Ulaya na Asia...yaani hiyo tabia wanayo hata sikumoja huwezi kukutana na
mznz nje ya tanzania ukamuuliza wwewe unatoka nchi gani akakujibu tanzania
wanapenda sana kujibu natoka ZANZIBAR...mpaka uwe hupajui au hujamuelewa ndo
atakwambia natoka Tanzania..

Hicho wanachokigombani si kosa ni haki yao
lakini hiyo ni dalili ya kutokuu...
Anonymous   |2010-08-12 12:53:48
hivi hawa wazanzibari kinachowafanya wajitenge ni hizo karafuu? seriously they
don't make sense...let them be nchi manake wako tofauti kama siyo wa-TZ
anyway...urojo mtupu...

eti nasikia wameambiwa zanzibar ikiwa nchi saudi
arabia itafungua visima vya kuchimba mafuta kwao....THERE ARE NO MAFUTA KWENYE
ARDHI YA ZANZIBAR DAMIT!!!!
mr s   |2010-09-03 13:23:28
Hi Mange
Sorry hivi hawa watu wanaotaka kuiizungumzia kuwa Zanzibar si nchi
nafikiri wana matatizo ya akili. Coz Zanzibar ni nchi na ina Culture yake na
ustaarabu wa hali ya juu. ambavyo wenzetu hawana hata kidogo , leo utasikia mtu
kakatwa kichwa mara miguu. zanzibar hakuna vitu hivyo basi ujue kuwa kuna
ustaarabu. Just wait and ] give the next five years u will see Zanzibar will be
the Paradise of Africa........poleni wadau
Write comment
Name:
Email:
 
Website:
Title:
UBBCode:
[b] [i] [u] [url] [quote] [code] [img] 
 
 
:confused:8):lol::x:P:oops::cry::evil::twisted::roll::wink::!:
:?::idea::arrow::blink::dead::coffee::karate::gossip::hahaha::newpost::love::lips:
:no::nono::rofl::shrug::stop::tape::thumbsup::wail::waves::yahoo::yes:
 
Please input the anti-spam code that you can read in the image.

3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."

 
 
Find U turn Blog on facebook