|
KINA DADA HAWA SIWAELEWI..... |
|
Written by Mange
|
|
Wednesday, 04 August 2010 19:12 |
|
Mange habari za kazi .. Naomba wenzangu ,mnisaide mnisaidie kina dada hawa siwaelewi..mie ni mama nina mtoto mmoja naishi Dar. Nilikuwa na rafiki zangu ambao tunafanya nao kazi bahati mbaya tulitofautiana na mie kuamua kukaa kimya na kuangalia maisha yangu na family yangu.ila nikawa nawapa salamu kwa tabasamu jema tu ingawa waliyonifanyia ni makubwa kusadikika. Cha ajabu tangu nimeacha urafiki nao ni miaka 3 sasa imepita lakini kila wakikutana na mtu wa karibu yangu wananiongelea kwa maneno mabaya na kunichafua jina langu. Wakikutana na ndugu zangu wa karibu vivyo hivyo wananisema vibaya sana Mbaya zaidi hata kwa mme wang u wamekuwa wakiongea mambo ambayo hayapo kabisa na mme wangu kunambia niwe makini nao.Nikipita sehemu lazima waseme hata sielewi ni sababu gani inayowafanya wanifanyie hivyo Ingawa wao tabia zao ni zile leo wako na mwanaume huyu kesho yule mradi maisha yaende Nifanye nini mie mwenzenu wananikosesha raha hawa.? Naomba email yangu usibandike asanet
|