U Turn Blog
PHOTO OF THE DAY.....
Written by Mange   
Monday, 08 February 2010 20:13

 
NAPATAJE RAHA?
Written by Mange   
Monday, 08 February 2010 15:34

Ni jinsi gani mwanamke unaweza kuongeza stimulation kwenye "Clitoris" yako when getting intimate with your partner? Mimi nina upungufu mmoja kwamba nikiwa kwenye tendo hilo, siwi stimulated during intercourse ila mtu wangu akiwa nje. Je ni nini nahitaji nifanye kama ni chakula gani cha kula, au vitamins au kingine ambacho nifanye ili kuongeza hisia kwenye Clitoris yangu. Samahani sana kwa kuchanganya lugha, sijaweza kutafsiri maneno mengine kirahisi ( you're more than welcome kunitafsiria ili wadau wako wote watoe maoni yao)

Chantel - us

Kuwasiliana na uturn tuma email kwenda This e-mail address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it

 
WANAUME WA KIBONGO---MNATUONEA.....
Written by Mange   
Monday, 08 February 2010 15:33

Hi Mange,

 

Naomba kuchangia mada ambayo imekuwa ikijirudia mara kwa mara kuhusu “wanaume wa kibongo”.Nikiri kuwa sina hakika neno “wanaume wa kibongo” linamaanisha Watanzania pekee au Waafrika kwa ujumla au Weusi (Blacks) wote.Ila kwa madhumuni ya mjadala huu,nitayumkinisha kuwa walengwa ni wanaume wa Kitanzania.

 

Pengine mtazamo wangu unaweza kuathiriwa na ukweli kuwa nami ni “mwanaume wa Kibongo” (Mtanzania).Hata hivyo,nitajitahidi kuepuka kujipendelea (subjectivity).

 

Kama nilivyopata utata kwenye neno “wanaume wa kibongo” (na hivyo kutumia dhana ya Watanzania) najikuta kwenye utata mwingine kuhusu neno “wanaume wa Kizungu”.Je linamaanisha watu weupe (Whites)?Au watu wa “dunia ya kwanza”/nchi za Magharibi ikijumuisha na weusi/non-Whites waliozaliwa huku?Je “wazungu” hao wanajumuisha pia wale wanaotoka “Ulaya iliyochoka” kwa mfano Ulaya Mashariki-ambapo baadhi yao wanalazimika kuja kutafuta maisha bora Ulaya Magharibi na kwingineko?

 

Tukiweka kando utata huo wa maana inayokusudiwa, kuna suala jingine ambalo ni muhimu kuliweka wazi.Nilipokuja Ulaya mara ya kwanza, nilikuwa na picha ya “wamisionari” –watu walioacha “raha” za kwao kwenda kuishi maeneo magumu kabisa kwao.Na nilikuwa na picha ya watu wenye upendo,huruma na wanaoguswa mno na shida zetu za kimwili na kiroho.

 

Lakini haikunichukua hata mwezi kugundua kuwa Ulaya nilokuwa naifikiria awali ina viumbe wa aina tofauti kama ilivyo huko nyumbani.Kuna wenye upendo na wenye chuki,kuna wenye busara na majuha,kuna wenye akili na machizi,nk.La kwanza nililobaini ni UBAGUZI.Sio tu wa rangi bali hata wa kipato.Wakati kimsingi jamii nyingi za kiafrika zimejengwa katika misingi ya ushirikiano,usawa na utu, kwa hawa wenzetu “ubinafsi” ( individuality, katika hisia chanya na hasi) una nafasi muhimu katika mafanikio au kufeli kwa mtu.Jitihada za mtu binafsi zina umuhimu mkubwa zaidi kuliko za ushirika/ujamaa.Hilo linaweza kuwa na uzuri wake lakini pia kuna suala la madaraja (classes) ambayo mfumo wa kibepari umeyaimarisha vizuri.

 

Na hili la madaraja ni muhimu sana katika kuzielewa jamii hizi.Kuna wale walioelimika na kuielewa dunia, na wengi wao-japo si wote- wanafahamu kwanini Afrika au Waafrika tuko jinsi tulivyo.Lakini kwa wale “waliokwepa umande”- japo si wote-kwao Afrika na Waafrika ni vitu vilivyopo duniani kimakosa.Ni katika kundi hili la pili ndipo kuna uwezekano mkubwa wa kukutana na “wapuuzi” wanaoamini kuwa Waafrika tunaishi maporini au kwenye miti huku tukizungukwa na nzi,tukijisaidia popote,na upuuzi mwingine kama huo.Kwa takriban mwongo mmoja niliokaa hapa Uingereza nimeshakutana na watu wa aina hiyo mara kadhaa na majibu yangu huwa “kama sie tunaishi kwenye miti je balozi wenu huko kwetu naye anamudu vipi kuishi kwenye mti?”.Ila mara nyingi huwa naishia kuwatukana tu.

 

Kuna suala la ubaguzi.Kwa hapa Uingereza,baadhi ya Waingereza wanakiri bayana kwamba “ubaguzi ni sehemu ya utamaduni wa baadhi yao...na ndio maana unaona Wakatoliki na Waprotestanti wanaendelea kupingana huko Ireland ya Kaskazini”.Wengine wanakwenda mbali zaidi na kueleza imani yao kuwa hisia hizo za kibaguzi zilichangia sana ukoloni wa dunia “ya watu wasiostaarabika”.Ni muhimu hapa kukumbushia angalizo kuwa wakoloni walikuwa haohao “wazungu walio bora kuliko Wabongo” japo hilo ni suala la kihistoria zaidi kuliko malavidavi.

 

Kwahiyo dada zangu wanaoamini kuwa “wanaume wa kizungu ni bora zaidi kuliko wa kibongo” wanapaswa kufahamu kwamba  miongoni mwa “wazungu” hao kuna wanaompinga Obama, si kwa vile hajatimiza ahadi zake bali tatizo ni weusi wake,kuna wafuasi wa British National Party (BNP),kuna neo-Nazis (vijukuu vya Hitler) na wengineo wenye “chuki binafsi” wakiamini kuwa vyanzo vya matatizo ya nchi zao sio Weusi tu bali Waasia na wageni wengineo.Nasisitiza,NI BAADHI.

 

Kama ambavyo huko nyumbani kuna wacha Mungu na washirikina,ndivyo ilivyo kwa “wazungu” pia. Kuna akina Mr Lawrie wa Mange wanaoangalia upendo,haiba,urembo na sifa nyinginezo za kibinadamu badala ya rangi ya binti,lakini pia kuna akina Nick Griffin, Jean-Marie Le Pen,nk ambao kwao rangi ya mtu ni kigezo muhimu cha utu/ “ushenzi” wake.

 

Labda swali naloweza kuwauliza dada zangu wanaohitimisha kuwa “wanaume wa kizungu ni bora kuliko wa kibongo” ni hili: je mama zetu waliolewa na wazungu kiasi cha kututengenezea familia bora zilizotufikisha tulipo sasa?Au je takwimu zinasemaje kuhusu idadi ya waume katika ndoa nyingi “zenye furaha” huko nyumbani?Japo nahofia kutoa takwimu pasipo utafiti lakini yayumkinika kusema takriban asilimia 90 ya waume kwenye ndoa “zilizotulia” huko nyumbani bado ni wanaume wa kibongo.Hapa simaanishi kuwa walioolewa na wasio “wabongo” hawana furaha na ndoa zao bali nasisitiza hoja kuwa kama mama zetu walikuwa kwenye furaha katika ndoa na baba zetu wabongo,sasa hoja ya “wanaume wa kibongo kutokuwa mwafaka kwenye ndoa” inatoka wapi?

 

Hivi wakati dada zetu wanaponyoosha vidole kuwashutumu wanaume wa kibongo wanajaribu japo kiduchu kujiangalia na wao wenyewe?Mbona hata huku kuna hadithi nyingi tu za watu kusaliti ndoa zao/mahusiano yao?Je Bill Clinton alipomsaliti Hillary kwa Monica Lewinsky alikuwa Mndengereko?Vipi kuhusu John Terry au seneta Edward Kennedy?

 

Katika sosholojia kuna theme inayohusu deviance (kwenye kinyume na taratibu zilizokubalika katika jamii husika).Hapo,baadhi ya wanasosholojia wanaamini kuwa umalaya ni uvumbuzi,yaani kwa mfano mwanamke mrembo anajua “anatakwa” na kuna walio tayari kutoa fedha kumpata kwa hiyo “anajipeleka sokoni,mwenye kiku kikali ale nyama”.Kuna wanaofanya hivyo kwa vile hali ya uchumi inawasukuma kufanya hivyo,na kuna wale wanaofanya hivyo kutokana na kufata mkumbo,huku wengine wakifanya hivyo kutumia uhuru wao wa kupenda chochote watakacho ikiwa ni pamoja na ngono.

 

Malezi,imani ya kidini na mchango wa wanaotuzunguka ni miongoni mwa mambo muhimu sana katika kutengeneza tabia ya mtu.Baadhi ya wansayansi ya jamii wanabashiri kuwa mtoto anayekulia familia ya mzazi mmoja (single parent) ana uwezekano wa kuwa single parent ukubwani kwa vile “kama baba/mama aliweza kunilea peke yake kwanini kie nishindwe?” (socialisation).Wapo pia wanaoamini kuwa mtoto anayekulia familia inayothamini umuhimu wa ndoa anaweza kuiga mfano wa wazazi wake na hivyo “kutulia” ukubwani.

 

Mwisho,naomba kuhitimisha kwa kusema kwamba ni mambo machache sana duniani ambayo yanatokea tu pasipo sababu. Kama kila mume/boyfriend wa kibongo “anakukimbia” pengine tatizo ni wewe na sio wao,hasa ikizingatiwa kuwa wao si mapacha.Lakini na muhimu zaidi ni la kiroho.Kwa sie tunaoamini Mungu,hakuna liwezekanalo kwa mwanadamu pasipo baraka za Mungu.Pengine kabla ya kukimbilia kulaumu “wanaume wa kibongo” ni muhimu kwa walalamikaji kutazama upya mahusiano yao na Muumba.Kuna ishu inayonong’onwa na baadhi ya wanaume (hususan walio nje ya Tanzania) kwamba dada zetu wa kibongo wanaondekeza tamaa za makaratasi na kubabaika lakini naomba nisiligusie kwa vile,again,tamaa kwa Wakatoliki ni mzizi wa dhambi.Kwa aliyemshika Mungu na kisha kupatiwa chaguo lake,chochote atachopewa kitakuwa ni mapenzi ya Mungu,hivyo masuala ya tamaa yatakuwa hayana nafasi.

 

Naweza kuwa siko sahihi lakini huo ndio mtazamo wangu.

 

Evarist Chahali

Glasgow,Uskochi.

http://chahali.blogspot.com

 
USWAHILI NI NINI????
Written by Mange   
Sunday, 07 February 2010 21:44

Few months ago a bunch of my friends and I were waiting for a Kenyan friend whom we were going to have dinner with, klock kept ticking and she wouldn't turn up at. A Swedish friend( who had been living in Tanzania for ages, and who is a fluent Swahili speaker)blotted out "Anna kishakuwa Mswahili. I as a Tanzanian, was not sure whether to laugh or be offended.. why did she not say "Anna kishakuwa Mkenya? why a Swahili? Is it that we are so bad or is it the expressions of "Uswahili" that we teach others turn to let us down? Uswahili ni nini?

 

When you reffer to someone else as a "mswahili", is it that you are putting a line between her class and yours? and if so, does it mean to say just because you are a little more educated, a little more exposed, then those who are below you need such a stamp as "Waswahili? Why?

 

Uswahili, Mswahili, Uswahilini ... Most of us have used those words.. You who call you fellow Tanzanian a "Mswahili regardless of his/her tribe, what does that make you, putting in mind that you are a Swahili speaker too . And what are the Zaramos suppose to feel about this since Swahili is their first and foremost a mother toungue? Aren't we putting them down?

 

I think this "Swahili" expression owe to be banned.. what do you think?

 Mika

 

 
WHAT ARE FRIENDS FOR??????
Written by Mange   
Sunday, 07 February 2010 21:21


Theo, Sophie and Chaya....


Adeline..


all of us at the Fish Bar...


Kisa, Jaki and Joselene


Mwammy....


Adeline,Mwamvita,Julie,Kisa,Sophie,Chaya and i....


What a great evening it was…just met up with the girls, for a little bit of laughter and good time.

Talk a bit about our lives and and basically just be there for one another…

Indeed a great evening it was..

I LOVE U ALL MY GIRLS….I REALLY NEEDED TO GET OUT OF THE HOUSE….

 
FLAVIANNA ATTENDS AFRICAN WILDLIFE FOUNDATION DINNER.
Written by Mange   
Saturday, 06 February 2010 20:29


Flavvy and Russel Simmons kama kawa....


Flavianna and fellow model Veronica Varekova


All smiles...


Representing Tanzania...Doing Big things... we love u Flavvy....


A true Tanzania Beauty....


African Goddess....


stavros

On the 3rd of February 2010 ,Flavianna Matata attended the Hublot and African wildlife foundation Dinner at American Museum of natural History –African Mammals Room in New York.

You Rock Flavvy, u-turn tunakufagilia sana….

 
10 signs he's not the one....
Written by Mange   
Friday, 05 February 2010 17:52

10 SIGNS HE's NOT THE ONE

Some people say they "just knew" that they were dating their future spouse. But what about the rest of us? What happens when you're not sure if he's The One? If you're considering long-term commitment or marriage, it's time to ask yourself some tough questions. Below, 10 signs that may indicate he's not for you.

1. You have a list of things he needs to stop doing/saying/wearing if he wants your relationship to work. If you're fixating on his flaws, he's either not the one you want or you're not ready for a serious relationship. Cutting him loose allows you time to grow and gives you the opportunity to meet a guy whose flaws you can embrace -- or at least accept.

2. You don't trust him. A small dose of jealousy can be healthy, but if you're hacking into his email account, and going berserk when he goes out without you, something's wrong. If there's something about him that truly warrants your distrust, then perhaps he's not the right one for you.

3. You avoid conflict at any cost. Fighting is healthy. And, when done right (in the non-accusatory, rational sort of way), it can be a great way to air grievances, fix problems in your relationship, and come to a deeper understanding of each other. Ignoring problems is not the same as having no problems at all... even if it looks that way.

4. When you're sad, you don't turn to him for comfort. When you're a giant ball of tears and snot, do you lock yourself into the bathroom so he can't see you at your worst? If you're worried about scaring him away, one of you isn't ready for total commitment. Mr. Right should make you smile through your tears and be a calming, not stressful, presence.

5. One of you is struggling with an addiction. He's sweet. He's exciting. He loves you very much. But he loves his alcohol habit or his weekly gambling fix more. Don't fool yourself into thinking that you can change him or that your relationship will be strong enough to withstand the heartache that addiction will inevitably bring. An addict may be able to change, but he'll do so on his own terms.

6. You can't really imagine him as the father of your children. Ask yourself: Would he make a great parent? Is he financially responsible? Would he be an equal partner in your future together? If you have doubts, he's probably not the one.

7. Your long-term, non-negotiable goals in life are incompatible. You want kids; he doesn't. You go to church every week; he's an atheist. He lives in the country and doesn't want to move; you can't imagine ever leaving the city. Superficial differences can be overcome, but differences in basic values are harder to smooth over. Ask yourself: "Would I be willing to compromise on this?" If the answer is absolutely not, you may not be right for each other.

8. You don't respect each other. He puts you down in front of your friends and complains about you to his parents. You roll your eyes when he talks because there's just something about him that embarrasses you. A relationship without respect can't sustain itself.

9. You're not attracted to him. Physical intimacy is a hugely important component of a romantic relationship. If he doesn't do it for you, he's probably not your best long-term match.

10. On paper he seems great, but you have this strange feeling... Don't ignore your gut. You may get along on a superficial level, but if your instincts are telling you he's not the one for you, listen. That little voice inside your head does not lie.

Louis


 
FLASHBACK FRIDAYS-MISSY - SHE IS A BITCH.
Written by Mange   
Friday, 05 February 2010 16:54

">

 
BREAKING NEEEEWS...LOL...
Written by Mange   
Thursday, 04 February 2010 20:45

Haya  wadau wa u-turn story hii fresh out of the oven dakika tatu haina

Kigogo mmoja (jina kapuni) anaejulikana vizuri mjini hivi sasa yupo njiani kummwaga mke wake mpya aliemuoa mwaka jana baada ya kumfumania laivu akifanya mapenzi na kijana mdogo  (jina kapuni) anaefanya kazi kwenye kampuni ya  mgodi nchini.

Kigogo huyo alikuwa amempandisha chati mke wake baada ya kumtoa kwenye shida na kumweka kwenye jumba la dhamani na kumnunulia vitu vya dhamani na kumlelea wanae.

Binti aliendelea kula  uroda na kijana huyo wa mgodi mmoja maarufu (jina kapuni) bila kujua kwamba Kigogo huyo anae mueka mjini amemuekea security kali ya kumfatilia .

Kina dada acheni tamaa, mnapenda kuwa na vijana wa umri wenu sasa kinachowapeleka kwa vibabu vizee visivyoweza kuwaridhisha ni nini?

Mie namsubiri kwa hamu huyu dada arudi mtaani ,bora yamemkuta ya kumkuta manake amekuwa na dharau sana na alisahau alipotoka.

MDAU, MASAKI

 
HABARI YA MSIBA.....
Written by Mange   
Thursday, 04 February 2010 19:42

Binti wa Marehemu Rashid Kawawa , Habiba Kawawa amefariki  jioni ya  Leo siku chache kabla ya arobaini ya baba yake katika hospitali Ya Taifa ya Muhimbili majira ya saa kumi na Mbili Jioni….

Msiba upo nyumbani kwa Marehemu Habiba huko Tegeta

May Her soul rest in peace….

 
<< Start < Prev 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 Next > End >>

Page 1 of 39
 
ADS Only